Wednesday, January 11, 2006

NANI KAWALOGA WAANDISHI WA HABARI!

Kichwa cha habari hata kisikuchanganye, mara nyingi siku hizi nimekuwa nishangazwa na waandishi wetu wa habari na hasa namna wanavyoripoti habari za mafanikio ya kiuchumi kwa watawala wa tanzania
Kinachonisumbua ni kuona kwamba utawala wa Mzee Mwinyi hauongelewi kabisa na kinachotukuzwa ni mafankio ya Nyeere na Mkapa kwisha.

Hivi ninyi waandishi mnajua namna maisha ya Watanzania yalivybadilika wakati wa mzee Ruksa au mnasukumwa na mapenzi binafsi kwa viongzi hawa, Hebu tizama hata daraja la Ndndu linaitwa daraja la Mkapa hii ni haki kweli?
Hivi ni nani anastahili pongezi kwa kuwepo kwa daraja hilo ni Mwinyi au Mkapa?
Hivi bila Mwinyi kumuibua rais wa sasa Kikwete kuna mtu angemjua kweli hebu tuache chuki binafsi kama ni suala a kukusanya kodi kidogo wakati wa ruksa mbona sasa kodi inakusanywa kubwa lakini hakuna kilichobadilika zaidi ya vitu kuwa juu na maisha kupanda kwa kila sehemu.
Sipendi niukubali msemo wa kwamba watanzania hatuna utamaduni wa kusoma si magazeti tu na vitabu lakini kama mwandishi hana falsafa kuna umuhimu wa kusoma kazi yake na hata kama anaiandika kwa mapenzi binafsi bla kujali nini jamii inafikiria

No comments: