Wednesday, January 11, 2006

Mara baada ya mwanguko mkubwa wa uchumi huko Marekani mwaka1930, Marekani chini ya rais wake Roosevelt, ilianzisha mpango kamambe wa kufufua uchumi wake uliojulikana kama Marshall Plan.
Moja ya mipango mingi ya kufufua uchumi nchini humo ulikuwa ni mpango wa uliopewa jina la mabadiliko katika sekta ya kilimo chini ya sheria za nchi. Katika mpango wa ufufuaji na uboreshaji wa sekta ya kilimo mkazo ulitiliwa katika utoaji wa mikopo na ruzuku kwa wakulima.
Mpango huu ulipofanikiwa mara baada ya miaka mitano mafanikio yake ni haya tunayoyaona leo. Soko lote la bidhaa za kilimo marekani amelishikilia.
Tanzania na mamlaka yake imekuwa ikiimba kila siku tangu tupate uhuru kwamba kilimo ndiyo uti wa mgongo wa taifa. Kauli mbiu na maazimio mbalimbali ya serikali yanasisitiza kuwa kilimo ndiyo kitaondoa umaskini katika nchi yetu.
Kwa ukweli hakika ni kuwa asilimia 80 ya watanzania wanategemea kilimo na kiasi hicho cha watu ni maskini wanaoishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku. Idadi kubwa ya watu hawa wote wanalima mashamba madogo vijijini.
Ukiiangalia Tanzania na ardhi yake bora ambayo kwa kiasi kikubwa haijatumiwa kwa ukamilifu,ukaangalia na idadi ya watu waliomo utaona kwamba endapo kilimo kitapewa kipaumbele basi kilimo ndiyo silaha kubwa ya kukabiliana na adui, umaskini.
Mpaka sasa wakulima wadogo wa Tanzania hawajawezeshwa ili kuondokana na shuka kubwa walilofunikwa lililogeuka kuwa tunu kwao,umaskini. Kuwezeshwa huku kwa mkulima mdogo hakuwezekani kwa hotuba tamu za kwenye majukwaa ya siasa na semina kwa warasimu kilimo bila ushirikishwaji wa wakulima na utekelezwaji wa maamuzi.
Mkulima wa Tanzania anahitaji misaada mingi ili kumwezesha ambayo wenye mamlaka wakiacha u-mimi, mkulima mdogo wa nchi hii atainuka na hata kuweza kushindani katika soko na wakulima wa nchi nyingine ambako mkulima anathaminiwa na kupewa kila aina ya msaada.
Ili kumwezesha mkulima wa Tanzania haina maana ya kwamba mkulima huyu apewe fedha za bure. Hapa ninamaanisha kwamba mkulima wetu apewe mikopo atakayopaswa kulipa pindi uuzaji wa mazao unapoanza. Ni mikopo tu ndiyo iliyotumika na inatumika katika kuondoa umaskini kwa wananchi katika nchi kama Mali na nyingine.
Jitihada nyingi za kuleta maendeleo zinazoonyeshwa na serikali yetu zinafaa sana. Lakini kwa upande wangu pamoja na kujenga madaraja na barabara nzuri

No comments: