Saturday, January 28, 2006

HAKUNA HAJA YA KUIGA KILA KITU KUTOKA NG’AMBO
Na: Obe M. Mashauri


Kuiga kitu ni ile hali ya kufanya kitu kwa kuona vile mwenzako alivyofanya. Ni kitendo ambacho huwa kinafanyika kwa siri lakini baadaye mgezaji huonekana na mwanzilishi hujulikana na kuheshimiwa.
Si vibaya kugeza kitu ambacho kitaweza kuleta unafuu fulani katika jamii. Mfano, kuiga ufundi wa kutengeneza trekta ni kuzuri kwani kutaleta unafuu kwa jamii ambayo muigaji anaishi. Kuiga teknolojia nako hakuepukiki kwani wote wanajamii wanahitaji teknolojia kwa maendeleo yao.
Kuna mambo mengine ambayo mtu ukiiga wenye busara zao watakuona punguani, chizi. Uigaji huu wa kishenzi mara zote hushusha utu wa muigaji, japo yeye hujiona ameendelea kwa kuiga hata vile vinavyopingana na utamaduni wake.
Utamaduni ni yale mazoea ya kale yasiyobadilika wala kugeuzwageuzwa. Kila mtu ana utamaduni wake ambao ameurithi toka kwa waliomtangulia kuona jua. Taifa nalo lina utamaduni wake. Wazungu wanao wao, waarabu pia, nasi waafrika tuna utamaduni wetu ambao tumekuwa nao kwa miaka mingi tu.
Inashangaza sana kuona waafrika tumekuwa ni mabingwa wa kuiga tamaduni za ng’ambo. Utamaduni wa mwafrika unapotea na sasa kinachonekana ni ule ustaarabu wa ng’ambo. Fahari yetu tunaizika na kukumbatia vitu tusivyovielewa mwanzo na wapi vinakwenda, sisi tunachojua ni kuiga tu.
Hapa sina lengo la kuongelea uigaji wa sayansi na teknolojia au vitu vya namna hiyo. Naongelea kuhusu utamaduni na ustaarabu wetu katika mavazi, maongezi na lugha, kula, mapenzi, dini na kuabudu. Vitu hivi waafrika tunavipoteza na kutokujali kwetu kunatufanya tuone vitu vyetu ni vya kishenzi.
Vijana watanzania wa karne hii tumekuwa ni mabingwa wa kuiga karibu kila kitu kinachofanywa na wazungu hasa wa Ulaya na Amerika ya kaskazini. Mitindo ya uvaaji, kuongea, kutembea na mingine tunaiga toka pande hizi.
Vijana ambao wengi tumebahatika kupata elimu japo kidogo tumekuwa ni mabingwa wa kuiga karibu kila kitu kutoka ‘majuu’ kwa mabepari hawa waliondelea. Haishangazi kukuta siku hizi vijana wanashindwa kuongea lugha zao za kuzaliwa au lugha yao ya taifa kuibolongabolonga.
Kijana anataka na anapenda kuongea lugha ile mzungu aongeayo si kwamba kijana huyu hana lugha yake, ni kule kutaka kujionyesha kwamba amesoma na kuongea lugha yake anaona ni kujishushia hadhi!
Ukitazama mahojiano yanayofanywa katika luninga na redio zetu utakuwa shahidi wa kuona vijana wanavyoikologa lugha yetu. Wanaongea ‘kiswa-nglishi’lugha isiyoeleweka kwa urahisi kwa jamii kubwa. Sasa sijui huku ndiko kutafuta maendeleo.
Kwa suala hili sitaki niamini kwamba kuelimika kwa mtu mweusi ni kuacha kuongea lugha yake. Kuelimika kwa mtu ni safari ya mtu huyu kuleta mabadiliko katika jamii yake na si kuharibu ustaarabu wa jamii yake.
Lugha yetu (ukiacha lugha zetu za kwanza)ya taifa ni muhimu sana kwa kila mtu wa nchi hii kuiongea kwani ni kitambulisho cha utaifa wetu. Inashangaza sana tunapong’ang’a na lugha tusizozijua vizuri kana kwamba hatuna lugha inayotuunganisha.
Tunaonekana ni watumwa kwani hapa mataifa yenye lugha tunazozing’ang’ania yajiona kama ndio yametusitaarabisha. Wakoloni walitukuta na lugha zetu na nyingine kubwa tu zilizotuunganisha. Swali hapa je, wasingekuja wakoloni na wafanyabiashara ya watumwa sisi tusingeweza kuwasiliana?
Ni jukumu la kizazi hiki cha vijana kujitoa muhanga kuhakikisha kwamba ustaarabu wa mwafrika hauharibiwi na vitu vya kishenzi kutoka ng’ambo. Kuongea lugha yako hakumfanyi msomi mswahili apoteze usomi wake ila kutamfanya aiboresha lugha hii iendane na wakati bila kuiharibu.
Majina yetu ya kiafrika sasa tunayakataa, tunayaona kama mkosi fulani. Tunatamani na tunataka tuitwe kwa majina ya kizungu ili tuonekane wastaarabu na hata tusio na dhambi. Nilihudhuria misa katika kanisa moja la Tabata college, mchungaji aliyehubiri alisema kwa watu kuitwa majina ya babu na bibi zetu waliofariki basi tunarithi hata dhambi zao! Huyu ni mtu anayechunga kondoo wa Bwana anayeamini majina ya koo zetu ni laana!
Majina tunayoyatamani ni yale ya wapelelezi na maharamia wa kizungu au wa kiarabu waliokuja kunyanyasa na kutuharibia nidhamu yetu. Mtu akiitwa kwa jina la ukoo wake si ajabu kuulizwa kama hana jina jingine la kikristo au kiislam! Majina ya kizungu au kiarabu tunayaona kama ni majina ya kistaarabu, yasiyo na dhambi kama anavyoamini mchungaji huyu. Tunatamani kuitwa majina ya watu wauaji, waasherati na mengine ya waovu kisa tu yameandikwa kwenye vitabu vya dini.
Suala jingine ambalo tumekuwa tukiiga sana ni dini na ustaarabu wa kuabudu. Itabidi ikumbukwe kwamba kabla ya wakoloni kuja, waafrika walikuwa na bado wana dini zao na ustaarabu wao wa kuabudu. Walikuwa wote wakimwabudu Mungu mmoja ambaye alikuwa akijulikana kwa majina mbalimbali lakini ni yule yule. Kuna walomwita Mulungu, Ngai, Katonda na majina mengine kutokana na lugha zao.
Bahati mbaya sana mawazo yetu yamegeuzwa ili kukubali kile mkoloni alichokuja nacho ili kututawala, ametupa dini yake. Tuna meza chochote kile anachotafuna na kutema vitamu vyetu na kuviita vya kishenzi, havifai kwetu sisi!
Wakoloni(mzungu na mwarabu) walikuja na kudai kwamba Mungu wao ndiye wa kweli. Mungu wetu waafrika, wakoloni wamemlinganisha na shetani na roho wake wameitwa mapepo! Kwa kutojua malengo ya wakoloni tumeacha dini zetu na kukumbatia dini mpya. Zinazotukana asili yetu.
Ni uongo wenye kutu kwamba waafrika hatukuwa na dini wala hatukumjua Mungu kabla ya wazungu na waarabu kuja kutupora utu wetu na kumtangaza ‘mungu’ wao! Kwa kulishwa ujinga na wakoloni hawa waafrika hatujui kuhusu Osiris mtu aliyeishi Misri (KK)aliyekufa na kufufuka. Huyu alikuwa akiabudiwa sana huko Misri
Ukristo ulipoletwa na wamisionari ulikuwa na jukumu la kuwa fundisha wenyeji imani chovu ili watawale bila maswali. Uislamu nao uliletwa ili tu kutimiza matakwa ya wachache waliokuwa na uchu wa kutaka kutawala. Wanadini wote hawa hawakufundisha theolojia ila tu walifundisha imani haba ya kutokuhoji. Tumebaki kuwa mabingwa wa kutetea dini hizi bila kuzijua malengo yake.
Dini hizi ngeni watu wanaziona ni bora sana na kuwapa majina ya kishenzi wasiozifuata. ‘Wapagani’ na ‘makafiri’ ni matokeo ya dini hizi zinazoonekana kama za wasomi wasiohoji. Dini hizi mara nyingi zina shawishi na kupenda vita, na kubaguana hizi ndizo tunazozikumbatia tukibusiana sisi kwa sisi!
Fujo nyingi zinatokea barani kwetu, sababu kubwa ikiwa ni dini hizi kutaka aidha kujitanua au kujionyesha kwamba ni bora. Mbaya zaidi maafa haya yanawakumba hata wasiozifuata. Mambo haya hayakuwahi kutokea na wala kuletwa na dini za mababu zetu zilizohimiza kujituma, nidhamu na upendo kwa watu wote. Sasa hapa tujiulize dini ipi ni bora
Kwa kutambua ukweli wa mambo kuhusu uafrika sasa baadhi ya wanateolojia akiwemo ‘fadha’ Mwanampepo wana kitu kinachojulikana kama ‘Kuitamadunisha Injili’ na kadri siku zinavyokwenda basi ni dhahiri kabisa waafrika watarudi kwenye dini zao zisizoshawishi mauaji na zisizotaka matabaka na kubaguana
Msomi Russell aliwahi kusema mwanzoni mwa miaka ya 1940 kwamba “mavazi na mitindo inayoonekana Ulaya mwafrika huiga bila kujiuliza na kwa imani yote”. Ukitazama kwa umakini utaona kwamba mavazi yetu waafrika yanaendana sana na hali ya hewa ya bara letu. Mavazi yetu ni mazuri kwa hali yetu.
Tunaiga uvaaji ambao si tu kwamba unatutesa kwa joto lililopo kwetu bali unatufanya tusionekane wastaarabu kwa jamii yetu. Sehemu nyigi za bara la Afika ni za kitropiki, joto haliepukiki. Kutokana na kuiga mavazi na uvaaji kutoka ng’ambo utashangaa kukutana na ‘msomi’ mchana wa jua kali akiwa amevaa suti kali na nzito. Joto na suti kweli jamani au ni kuiga tu. Jasho mwili mzima!
Mavazi ya vijana ndiyo yanayochosha zaidi. Kijana mzuri wa kiume unakuta amevaa sarawili ambayo ameivalia chini ya kiuno eti wanaita ‘kata K’ na anapita barabarani akitembea kwa madaha. Watoto wa kike nao suruali zinazobana na vijinguo vinavyoonyesha kitovu na ‘upindo wa kufuri’ ndiyo vimekuwa fasheni. Mavazi haya si tu kwamba yanadhalilisha bali yanashawishi na kuongeza hamu ya ngono ambayo madhara yake tunayajua kwa maendeleo ya taifa na bara letu.
Mavazi haya tunayoyaiga hasa sisi vijana hayafai na yanashusha hadhi ya kijana katika jamii yake. Kijana wa kiafrika ni mtu muhimu katika kuleta maendeleo ya jamii yake. Ni budi akajiheshimu kwa kuvaa nguo zinazomsetiri na kumwonyesha kwamba ni mstaarabu.
Kwa kutovaa mavazi mazuri yenye staha vijana wengi wamejikuta wanagharimika aidha kwa kuhisiwa ni wezi au malaya. Mavazi mazuri na uvaaji ulio sawa humjengea mtu hata kama ni mgeni kupata mapokezi mazuri ya kirafiki. Ni mara chache sana kwa mtu aliyevaa vizuri kuhisiwa kwa wizi au uchangudoa barabarani (japo wapo wanaovaa vizuri na wanatabia hizi.
Mwaka 2002 tumeshuhudia kuzaliwa kwa Umoja wa Afrika. Karibu viongozi wote wake kwa waume walihudhuria wakiwa wamependeza sana kwa mavazi yao mazuri. Wanawake walipendeza zaidi kwa nguo zao zilizowaonyesha kwamba hakika ni Waafrika. Hii ni tofauti kabisa kwa viongozi wanaume ambao (si wote) walikuwa ndani ya mavazi ya kimagharibi, suti nzito za gharama. Hivi kweli hatupenda kuvaa nguo zetu zenye kuonyesha fahari yetu!
Wengi wataona kama ni kukurupuka endapo mtu atasema ustaarabu wa binadamu ulianzia Afrika! Kuna ushahidi unaoonyesha kabisa kwamba kabla ya maharamia kuja kwetu( Afrika)maeneo mengi yalikuwa yamestaarabika kiasi kwamba majahili hawa waliiga ustaarabu wetu. Mwanahistoria Walter Rodney anathibitisha hili katika klitabu chake kinachoitwa ‘How Europe Underdeveloped Africa’
Suala jingine ambalo ni muhimu katika maisha ni urafiki na mapenzi kwa vijana. Tamaduni zetu waafrika ni tofauti na tamaduni za wazungu au waarabu, tunachopenda sisi si lazima wao wafuate na wakipendacho wao hawatulazimishi kufuata.
Ni ukweli usiofichika kwamba taifa bila vijana waadilifu si lolote. Vijana wakipotoka basi jamii itegemee kilio kwani hakuna maendeleo yoyote yatakayopatikana ikiwa nguvu kazi ni butu. Wazee ni muhimu kwa kuelekeza na kutoa ushauri na vijana ni watekelezaji wa shughuli zote za jamii.
Vijana wengi sasa wanakazana kuangalia tamthilia za kigeni zilizojaa maudhui mabovu kwa vijana wetu. Mara nyingi michezo hii huonyesha maudhui ya mapenzi kwa wahusika wenye umri mdogo. Nasi twataka kuiga kila sehemu ya tamthilia hii. Hadithi za mababu zetu hazina nafasi tena, sasa mambo yote ni luninga na video.
Mapenzi si kitu kibaya, kwani yalikuwako tokea mwanzo. Muhimu hapa ni jinsi mapenzi haya ya kuiga kwenye luninga yanavyolighalimu bara hili. Vijana wamejiingiza kwenye ngono(si mapenzi)wakiwa na umri mdogo kwa vile tu wameona mhusika kwenye tamthilia anafanya mapenzi ilhali ana umri mdogo.
Vijana tumekuwa si wakweli na mpaka mtu anapofikia umri wa kuoa tayari huwa na namba kubwa ya wapenzi aliokwisha fanya nao ngono. Hiki kitu hakikuwepo kabla na yeyote anayetaka kubishi aweza bishi kwa kuwa ubisha yaweza kuwa hulka yake. Kijana ana miaka 19 na tayari ana ‘wapenzi’saba. Hii inatisha!
Hapo juu nimesema kwamba kila mtu ana utamaduni wake, tamthilia, sinema na michezo ya kuigiza toka nje ya bara hili huonyesha utamaduni wa sehemu hizo. Kuiga kile kinachoonekana ni juu ya mtazamaji na akili yake.
Jamii zetu nyingi haziruhusu mapenzi kwa vijana waliona na umri mdogo. Ili kijana awe na mchumba alitakiwa kuwa na uwezo wa kujitegemea yeye mwenyewe, hii ina maana kwamba kijana anaanza kumjua binti wakiwa na umri ufaao kwa mapenzi na si ngono.
Ngono zisizo salama zinazofanyika kabla ya wakati zina madhara makubwa ambayo kila mwanajamii anayaona. Mimba zisizopangiliwa ni nyingi tu magonjwa ya zinaa sasa yanawakumba zaidi vijana wasiooa. Haya yote ni madhara ya kuiga.
Zamani vijana wote kwa jinsia zao walikuwa wakikaa na wakubwa zao na kupata nasaha mbalimbali kuhusu maisha. Kutokana na mwingiliano wa kijamii na mabadiliko ya kiuchumi kila mtu anahangaika kupata chochote, muda wa kuongea na vijana haupo na kama upo hautumiki ipasavyo. Ndivyo tunavyopotezana.
Kazi huonyesha utu wa mtu, yeyote asiye na kazi katika jamii huonekana mvivu na mnyonyaji wa nguvu ya jamii. Ni ukweli kwamba kwa sasa kuna tatizo kubwa la ajira na ukosefu wa mitaji. Hili ni jambo ambalo liko chini ya serikali na wananchi wake. Watu kukosa kazi ni tatizo ambalo linaangukia mikononi mwa watawala. Kukosa kazi kunafanya watu kuiga yale yanayoonekana kwenye sinema.
Wimbi la ukabaji na uporaji linaloonekana sasa katika mitaa yetu ni matokeo ya kukosa kazi na hivyo kuiga yale yote yanayoonekana kwenye senema za kimagharibi. Jambo hili ikiwa halitapatiwa ufumbuzi mapema basi kitakachokuja kutokea wakumlaumu atakuwa ni kiongozi aliye madarakani na watendaji wake walioshindwa kuona tatizo hili kwa kuwa wao wameshiba.
Ni vizuri tukiwa na watu tunaojitegemea na kujitawala! Tukawa ni watu wenye maamuzi ya kulinda na kuhifadhi historia na utu wetu. Ustaarabu na utu wetu tusiukane na kuuita wa kishenzi. Taifa au mtu asiye na utamaduni ni kama mti usio na mizizi (kama upo!).
Tamaduni, jadi, mila na utu wetu waafrika hauhitaji ‘rafiki’ mgeni aje kutoka nje atuambie sasa na tuache kuiga tamaduni mbovu kutoka kwa rafiki zetu.
Kulinda na kutunza kumbukumbu zetu hakuhitaji ushauri toka sehemu yoyote. Ni jukumu letu kulinda kilicho chetu na kuiga kile kinachotufanya tuonekane wapumbavu mbele za watu walioamua kuhifadhi vilivyo vyao.
Maendeleo ya sayansi na teknolojia pamoja na utandawazi yasiwe chanzo cha sisi kupotoka na kutaka kudandia gari kwa mbele. Madhara yampatayo mtu anayedandia gari lililo kwenye mwendo nadhani kila mtu anayajua. Je, na sisi waafrika tupate madhara haya?
Jibu la maswali haya tunalo nalo ni rahisi sana, halihitaji kutazamia kwa ‘rafiki’ jirani. Uwezo wa kulinda utu kama waafrika umo mikononi mwetu na ni sisi kuamua tu kwamba HAKUNA KUIGA UPUMBAVU.
Kiongozi wa mapinduzi wa Libya amewahi kusema kwamba “mzalendo anayekula chakula kisichozalishwa nchini mwake huyo anaukana uhuru wa taifa lake”. Hii ilikuwa mwaka1984 katika kuadhimisha miaka 15 ya mapinduzi.
Kauli hii ina mashiko ikitafakaliwa kwa umakini ni kauli inayohitaji kila mtu atumie kile alichonacho bila kukidharau. Wote tukae chini na kukubaliana kwa kauli moja ya kwamba kuiga mambo yasiyoendana na sisi ni upuuzi.
Tuige vitu vitakavyoipatia jamii nafuu. Tuige teknolojia ambayo itatuondolea tatizo la kilimo cha kutegemea mvua. Viongozi wahakikishe pato la wanaye muongoza angalau lina eleweka. Ufisadi utokomezwe na watu/ wananchi waishi kwa raha na uhakika wa kupata mlo kamili.
Tuondokane na uigaji ambao huwafanya viongozi wajali matumbo yao tu. Tusiige ufisadi wa kuuza rasilimali zetu muhimu kwa wajukuu wetu. Tuwajengee wajukuu wetu uchumi imara ili wasije tuona kama hatukuwa na akili timamu. Tutunze vyetu ili watoto wetu wasiyachape makaburi yetu viboko kisa hatujawaachia msimamo thabiti.

3 comments:

Anonymous said...

[url=http://firgonbares.net/][img]http://firgonbares.net/img-add/euro2.jpg[/img][/url]
[b]store softwares, [url=http://firgonbares.net/]buying software license[/url]
[url=http://firgonbares.net/][/url] best price for software adobe photoshop cs3 for mac student version
adobe imaging software [url=http://firgonbares.net/]tips for selling software[/url] 8 oem software
[url=http://firgonbares.net/]computer software to buy[/url] microsoft email software
[url=http://firgonbares.net/]windows vista software for sale[/url] find cheap software
educational software language [url=http://firgonbares.net/]windows xp download minutes[/b]

Anonymous said...

[url=http://hopresovees.net/][img]http://vonmertoes.net/img-add/euro2.jpg[/img][/url]
[b]nero smart start, [url=http://vonmertoes.net/]software retail stores[/url]
[url=http://bariossetos.net/][/url] buying adobe software good software to buy
buy antivirus software online [url=http://vonmertoes.net/]line software store[/url] where to sell software
[url=http://hopresovees.net/]kaspersky blocking google[/url] coreldraw 3d hollow cylinder
[url=http://bariossetos.net/]adobe creative suite 3 design premium trial download[/url] adobe acrobat 9 pro extended
educator discounts on software [url=http://vonmertoes.net/]discount microsoft office 2003[/b]

Anonymous said...

[url=http://bariossetos.net/][img]http://hopresovees.net/img-add/euro2.jpg[/img][/url]
[b]is oem software legal, [url=http://hopresovees.net/]windows vista background[/url]
[url=http://bariossetos.net/][/url] software microsoft office adobe photoshop cs3 support
quarkxpress free full download [url=http://hopresovees.net/]how to sell software online[/url] adobe photoshop cs3 extended
[url=http://bariossetos.net/]i buy dreamweaver cs3[/url] agent office software
[url=http://bariossetos.net/]adobe photoshop cs4 master editioncracked[/url] Pro 11
adobe photoshop cs4 upgrade [url=http://hopresovees.net/]winzip 12 crack[/b]