Monday, April 02, 2007

RVF: KILA MMOJA ANAJIDAI ETI YE'VEJETARIANI'

Homa inayoogopwa kabisa kwa sasa imeingia dar. Inaogopwa kwa sababu inapatikana katika kitoweo tena kitoweo chenyewe kikiwa ni nyama ya ng'ombe. Homa hii kitaalamu imepewa jina la Rift Valley Fever ama kwa kiswahili homa ya bonde la ufa.

Hapa chuoni kwa sasa kila mtu amejipachika 'urasi' kwamba yeye si mtu wa nyama bali ni matunda na mboga za majani. Ukienda kafteria chakula kinacholiwa sana ni ugali ama wali na mbogamboga ambazo hata hivyo zimepikiwa mafuta ya wanyama.

Labda tueleweshwe zaidi kuhusu hii homa, hivi haya mafuta ya wanyama hayana HBU

No comments: