Sunday, April 29, 2007

CHESII YAKARIBIA FAINALI YA UEFA

Klabu bingwa ya soka Uingereza majuzi iliweza kuilaza timu ya livapuli kwa bao moja bila majibu katika uwanja wake wa nyumbani Stamford Bridge.

Bao hilo lilifungwa na winga teleza Joe Cole baada ya kupata pande safi kutoka kwa mwanasoka bora wa Afrika na nyota anayeongoza kwa kupachika mabao katika primia ligi Didier Drogba.

Hii ni hatua kubwa sana katika kuelekea finali na endapo jumanne katika mechi ya marudiano chesii watashinda basi ndoto za Mourhino ya kutwaa kombe zitatimia.

Kumbuka kuwa nyota wa Ghana Michael Essien atacheza katika mechi hii japo kuna shaka ya mlinzi 'kavalo' amabye aliumia wakati wa sare ya ligi dhidi ya Bolton jana

No comments: