Monday, April 02, 2007

SULUHU KAMA USHINDI VILE......

Lilikuwa ni bao la kusawazisha liliofungwa kipindi cha pili muda wa lala salam ndilo lililobadilisha matokeo na kuiokoa timu ya chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere isiadhirishwe na chuo cha ustawi- Kijitonyama.

Mechi hiyo iliyofanyika katika uwanja wa MNMA ilishuhudia timu ya MNMA ikiwa ya kwanza kupachika bao lililofungwa na mshambuliaji mahiri Magesa dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza na hivyo kuamsha ari kwa wachezaji na washangiliaji waliokuwa wamejazana kwa wingi kuisapoti timu yao ambayo haina rekodi nzuri ya kushinda mechi inazocheza katika uwanja wake wa nyumbani.

Hatahivyo Ustawi walisawazisha kabla ya mapumziko. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Ustawi wakifunga bao 'tamu' la luninga lililofungwa na mshambuliaji mwenye jezi namba9mgongoni. Bao hili liliwachanganya wachezaji na mashabiki pia huku wakijikuta wakirejea kumbukumbu za timu ya taifa kufungwa na simba wa teranga. Lakini alikuwa ni Marijani aliyefuta ndoto za wageni kuongoza baada ya kusawazisha goli baada ya kupokea pasi safi toka kwa winga mahiri Joshua 'basopa'.

Mpira huu ulioshuhudia kazi kubwa kati ya mshambuliaji wa Ustawi na beki wa pembeni wa MNMA Allain, ulitawalaliwa na rafu za kimchezo huku mwamuzi akijitahidi kuumudu mchezo. Ustawi walipata bao la tatu baada ya kiungo mchezaji jezi namba14 alipounganisha krosi safi toka winga ya kushoto. Lakini ni Ayub Denge maarufu kama Jobe ndiye alieleta faraja kubwa kwa MNMA baada ya kufunga bao la shuti lililomshinda kipa wa Ustawi na kuleta furaha kubwa kwa mashabiki wa MNMA.

Hadi mwisho wa mchezo timu zote zilitoka nguvu sawa. Baada ya pasaka timu ya MNMA inataraji kucheza na timu ya IFM

Timu ya MNMA iliwakilishwa na
1 SWEDI
2 Allen (
3 Maximilian
4 MUDI
5 Father
6 RASHIDI
7 Baseke
8 Mungai
9 Hamad (Marijani)
10. Jobe
11 Magesa(Joshua)

No comments: