Friday, August 27, 2010

kundi la Wanaume (lililojiengua kutoka kwa kundi la Wanaume Halisi) linatarajia kuitambulisha albamu yake mpya itakayokwenda sambamba na uzinduzi wa Logo pamoja na tovuti yao kwa watu maalumu ndani ya kiota cha maraha kilichopo kati kati ya jiji,Savanah Lodge mnamo Octoba 25.

Akizungumza na Jiachie jijini Dar jioni hii kiongozi wa kundi hilo Rich One amesema kuwa baada kuikamilisha albamu yao yenye jumla ya nyimbo kumi,kwa sasa wanajipanga vyema kuitambulisha albamu hiyo itakayojulikana kwa jana la POA TUA, vile vile utakwenda sambamba na uzinduzi wa Logo na tovuti itakayokuwa na habari zao mbalimbali zikiwemo na kazi zao kama vile vyimbo na video zao.

"Tumeamua kuja na mambo mapya baada ya kimya kidoogo kwa wapenzi wetu,kama nilivyosema hapo awali albamu ina jumla ya nyimbo kumi,ambazo baadhi yake ni Poa Tu, Mapenzi Matamu, Apple, Moyo Wangu, Zaga Zaga na nyingine nyingi," alisema Rich One na kuongeza kuwa albamu hiyo imesheheni mahadhi tofauti tofauti kama vile Zouk, R&B pamoja na Hip Hop.

Rich One amesema kuwa ndani ya albamu hiyo amewashirikisha wasanii kadhaa mahiri katika anga ya muziki wa kizazi kipa,kama vile Chidi Benz,Kitokororo wa FM Academia,Hard Mad,Chiku Keto,Mh Themba na wengineo.

Kundi hilo linaloundwa na wakali akiwemo Athuman Yahya (A.Man), Juma Mbelwa (Juma Jazz), Karim Kaiman (Kakaman), Abdul Ally (Mzimu), Richard Shauri (Rich One) pamoja na David Mpangile (Da
Mama Salma Kikwete
NA MWANDISHI MAALUM, RUFIJI

WANAWAKE wanaokopa kutoka taasisi za fedha, wamekumbushwa kuzingatia masharti ya mikopo ikiwa ni pamoja na kuirejesha kwa wakati kuwezesha wengine kutumia fursa hiyo.
Akizungumza na kina mama wa wilaya za Mkuranga, Bagamoyo na Rufiji, mkoani Pwani, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, alisema kukopa fedha na kutozirejesha ni kukwamisha jitihada za wengine ambao nao wanazitaka kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.Mama Salma alisema kwamba, mtu anapokopa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi, ahakikishe anazitumia kwa kazi hiyo na sio vinginevyo.

"Kina mama wenzangu, mkopo ni mkopo, lengo lilokufanya uchukue mkopo ni mradi wa kujiletea maendeleo, usitumie fedha za mkopo kununua doti za khanga, huko ni kujisababishia matatizo bila sababu za msingi," alisema.

Alifafanua kwamba, serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani ilikuwa na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila Mtanzania, na fursa ya kupata mikopo, inalenga katika kuwezesha kauli mbiu hiyo kutekelezeka.

Mama Salma aliwasisitizia wanawake kuendelea kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) na VICOBA, ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kupata fedha za mikopo kwa ajili ya kuendeleza na kuanzisha miradi ya uzalishaji mali.

Kuhusu elimu, alisema mataifa yote yaliyoendelea, yamewekeza katika elimu ya watoto wao ndiyo maana serikali chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete katika miaka mitano yakuwepo madarakani, iliamua kujenga shule nyingi za sekondari na kupanua elimu ya vyuo na vyuo vikuu.
Huku akiwaomba kina mama hao kumpigia kura mgombea urais wa CCM Rais Jakaya Kikwete na wagombea wa ubunge na udiwani wa chama hicho katika uchaguzi mkuu ulipangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu, Mama Salma alisema miaka ya sasa siyo ya kupuuzia elimu.

"Nchi yoyote yenye mafanikio imewekeza vyema katika elimu ya watoto wao, nasi hatuwezi kubaki nyuma katika hilo, shule nyingi tumejenga kwa nguvu zetu na msaada wa serikali, lakini pia tunakabiliwa na changamoto nyingi kuziwezesha kuwa bora zaidi," alisema."Mkikichagua tena Chama Cha Mapinduzi kitafanya kazi hiyo kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi," alisema.
 
hebu angalia hapa kitu wanachokifanya,yaani washasahau kwamba barabara hiyo inatumiwa pia na watu wengine.na hapa ni lazima watakuwa walikuwa wanapiga soga tuu.
uandishi: Othman Michuzi | Tarehe: Wednesday, August 25, 2010
hii ndinga nimekutana nayo mchana wa leo katikati ya jiji la Dar ikiwa imeleta noma (kuharibika) huku jamaa wanaofanya kazi katika gari hilo za usafi wa mazingira wakiwa wamekaa juu ya taka hizo zilizomo ndani ya gari hilo huku wakipiga stori za hapa na pale kana kwamba wapo majumbani mwao vile,tena bila hata wasiwasi.
  


Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakiangalia Simba anayepita karibu na magari yao wakati warembo hao walipotembelea Hifadhi ya Ngorongoro kujionea wanyama na mambo mbali mbali yalipo katika hifadhi hiyo.
Baadhi ya warembo wanoshiriki mashindano ya Kumsaka Vodacom Miss Tanzania wakicheza ngoma ya Kimasai wakati walipokaribishwa katika Boma la wafugaji hao lililopo ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro wakati wakiwa katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya Utalii vilivyopo Mikoa ya Kaskazini, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani.
Baadhi ya Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakitoka katika nyumba za Tembe za wafugaji wa jamii ya Kimasai waishio katika Hifadhi ya Ngorongoro wakati wakiwa katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya Utalii vilivyopo Mikoa ya Kaskazini, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani.
Baadhi ya warembo wa Vodacom Miss Tanzania 2010 wakinunua shanga za kimasai kutoka kwa wauzaji waliopo katika Boma lililopo katika Hifadhi ya Ngorongoro wakati warembo hao walipotembelea hifadhi hiyo wakiwa katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya Utalii vilivyopo Mikoa ya Kaskazini, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani.
 
 
 
 
 

No comments: