Thursday, April 17, 2008

UTAJIRI WA CHENGE

Kama kuna jambo ambalo linaongelewa sana kwa sasa hapa kwetu Tanzania ni suala zima la utajiri wa Chenge ambaye aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali kwa kipindi cha miaka 10 katika zama za Mkapa.

Ni katika kipindi hiki ndipo taifa lilishuhudia uingiwaji mkubwa wa mikataba ambayo leo ndio inawasumbua watanzania.

Mikataba hii haikufungwa na kina chifu Mangungo bali ilifungwa na wasomi mahiri kabisa na wengine waliosoma vizuri katika vyuo vikubwa kabisa duniani na tena wakilipiwa na wanachi masikini kwa lengo moja tu kubwa, kuwatetea wananchi katika mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Lakini sasa tunachoshuhudia ni kinyume cha yale tuliyoamini, wale tuliowasomesha wamekuwa ni vinara wakubwa wa ufisadi na wamejaa viburi kiasi kwamba mtu anasema hawezi kuachia ngazi/madaraka kwa kelele za wananchi, swali langu hapa ni hili,

Hivi Mtanzania ni nani katika Tanzania!

No comments: