Friday, January 25, 2008

HE! UNAFIKIRI HII NDIO NJIA SAHIHI?

Wakati wananchi wa sehemu fulani hapa Tanzania waliposikia kuwa 'gavana' ametolewa katika nafasi yake, baadhi ya wanajamii walivamia mashamba yake kilometa chache nje ya mji mkuu wa kibiashara.

Mimi kitendo hiki ninakiona ni cha kipekee kabisa, yaani mtu anapigiwa simu kuwa waende wakagawane mashamba ya fulani kwa kuwa tu huyo fulani ni fisadi! Wapi tunakwenda.

Sina hakika kama yale mwimbaji maarufu na mwanaharakati wa Marekani Tracy Chapman aliyoimba katika REVOLUTION 'mapinduzi ya watu wa chini' yanatimia.

Je!, wasiosema wameanza kusema! au wasiosikia wameanza kusikia, na nini kitafuata endapo mikononi watashika kilichokaribu yao!

Tusubiri

No comments: