Friday, January 25, 2008

SAKATA LA BOT: WALIO KIMYA NAO WAMEKULA


Sidhani kama kuna yeyote mwenye uchungu na Tanzania anahitaji kuelezwa mwanzo wa mabilioni 133 yaliyotafunwa, kwa taarifa, pale kwenye benki kuu ya Tanzania. Kwa sasa kila mtu anamnyooshea mkono Ballali, gavana ambaye rais Kiwete ametengua uteuzi wake kama gavana.

Kwa maoni yangu, mimi nadhani mtu kama Ballali hawezi kuzitumbua pesa hizo peke yake hata kama angekuwa anakula kama funza. Kawaida ya funza huwa anakula na k****a wakati huo huo na ndio maana funza ni waharibifu wakubwa na mazao ya nafaka.

Hizi pesa zimeliwa na wengi, wengi tena sana ila kwa kuwa Ballali alimuonesha 'mungu' tumbo pale alipokanusha taarifa ya dk Slaa basi ndo leo umma umeamua kumuhukumu, na hakika hata kama atasafishwa vipi bado sisi tunamuona kama fisadi anayestahili kuhukumiwa na kufilisiwa kabisa na kama ndo ingekuwa katika zile nchi za kisoshalisti za kweli basi angeuawa hadjharani baada ya kuwa amewataja mafisadi wenzake.

Namtetea Ballali kuwa hizo pesa hajazila peke yake, amekula na wengi ambao wapo bado madarakani tena wanashikilia nyadhifa kubwa sana zinazowawezesha kusaini mikataba kwa niaba yetu huku wakitanguliza maslahi yao kwani hii ni kawaida yao. Tunaimba pamoja kijamaa wao wanacheza kifisadi.

Wengi waliokula wamekaa kimya huku wakijifanya hawahusiki na tena wengine bado ni 'wajumbe' wa bodi. Tunawasubiri hawa waseme kwa hiari la sivyo umma utawataka waseme wakiwa uchi

No comments: