Monday, November 06, 2006

WANAOMILIKI SILAHA WAKO TIMAMU!!!

Imetokea majuzi kwa mkuu wa mkoa wa tabora, mtoto wa mjini Dito amemuua kwa kumpiga risasi dereva wa daladala kwa kuwa tu jamaa aligonga gari la mhe. huyu lililokuwa likiendeshwa upande wa watembea kwa miguu. Hii ya kutembea kwenye service road si ishu yangu bali ninauliza hivi kweli kuna uhalali wa kiongozi wa serikali kama Dito kutumia bastola yake kumtaka dereva ashuke garini! na polisi wanatuambia eti ililipuka kwa bahati mbaya!

Naogopa sheria isije ikafumba macho. Tusubiri

No comments: