Asubuhi inapoanza na jua tamu kuchomoza basi pana shaka mchana wa jua unakaribia ukiita jioni kwa sauti kavu kama mtu asiyekunywa maji, na haya ndiyo Machweo yenyewe ambayo mtu hukaa na wenzake kutafakari nini amefanya kwa mchana na apange nini kwa kesho inayosadifiwa na nyota zinazoonekana kwa wingi
Wednesday, March 28, 2007
Niliyofundishwa kwamba walipokuja wamisionari hawakuja kufundisha juu ya Mungu, walikuja kushiriki kikamilifu ili kuhakikisha kwamba wazungu wanapata watumwa kwa namna yoyote ile. Walikuja wakiwa wameshika baibo na wakakiri kabisa kwamba wao ni wema na mungu wao anaruhusu utumwa.
Usishangae! Majuzi kanisa la Angilikana limekubali na kusikitishwa na kitendo chake cha kushiriki katika biashara 'haramu kwa kipindi hiki' halali ya utumwa kwa kipindi kile. Akiongea mjini Landani jumamosi wakati wa maandamano ya kuadhimisha miaka200 tangu bunge la Uingereza lilipopitisha sheria ya kuzuia biashara na utumwa wenyewe, askofu mkuu wa canterbury daktari Rowan Williams alisema kwamba kanisa linasikitishwa na hali ile na linapanga kulipa fidia.
Swali, Watamlipa nani
Wednesday, March 21, 2007
Unaikumbuka ile kesi ya wale jamaa waliomuua wakili Kapinga mnamo mwaka2002! Jamaa hawa walikaa rumande kwa muda wa miaka5 na hukumu ya kesi ilitaja kuwa walikuwa wakituhumiwa kumuua wakili huyo maarufu. Hawa hawakuonwa. Dito kaua hadharana na bado kamanda wa polisi anajaribu kutuaminisha kuwa bastola ilivyatuka kwa bahati mbaya! Amefanikiwa kwani mapema tu DPP aliibadili kesi toka mauaji mpaka kukusudia kuua.
Mahabusu wengi wenye kesi za namna ya 'mtoto wa mjini' wamekaa rumande kwa muda mrefu sana kwa kuwa tu 'upelelezi haujakamilika' (hawa si matajiri) jiulize jamaa waliotuhumiwa kumuua Kapinga hawakuona na yeyote lakini mahakama imewahukumu hukumu nzito kabisa. Dito, hadharani kabisa katoka ndani ya shangingi lake kashika bastola na kuifyatua ikimlenga dereva bado tunaambiwa eti hakukusudia kuua! Tunakokwenda siko.
Jiulize waziri mmoja anasimama na kusema kuwa kesi ya kigogo huyo imekuwa hivyo kwa sababu ana mawakili wazuri! mawakili wazuri ama kuna kitu kingine kilichoanzia kwa Tibaigana, mkurugenzi wa mashtaka na 'serikali'
Tunakokwenda siko na itafikia wakati wenye kutosikia watasikia na mabubu watasema, nimalize kwa kukumegea kipande ambacho mwanamuziki na mwanaharakati Tracy Chapman anasema katika wimbo wake 'Revolution'. Utafute na uusikilize utapata zaidi ya sauti nzuri na milio murua ya magitaa (mara nyingi hutumia gitaa tu)
Saturday, March 17, 2007
Juma hili linamalizika huku mawaziri wanaohusika na usalama na haki za raia wakishindwa kuwashawishi mahabusu amabo wamekuwa wakigoma sasa mpaka nao kesi zinazowakabili mahakama zitasikilizwa kwa haraka kama ilivyotokea kwa mtuhumiwa wa kesi ya kukusudia kuua ndugu Ditto amabye kesi yake imechukua miezi mitatu tu na sasa yupo nje kwa dhamana kwani kosa lake lina dhaminika ilhali mahabusu wengi wakiwa gerezani kwa takribani miaka10 mpaka 15 kesi zao zikitajwa tu bila chochote kuendelea.
Wamegoma!
Nawashangaa sana hawa mahabusu amabo wameamua kugoma ili kushinikiza kesi zao ziharakishwe kama inavyotokea kwa kesi zinazowakabili vigogo ama watoto wao ama watu maarufu. Kesi zinatofautiana na watuhumiwa wanatofautiana sana kwani hata binadamu wote si sawa japo katiba yetu inayoongozwa na mfumo wa ujamaa kutamka kuwa binadamu wote ni sawa.
Kesi inayoendelea ya mheshimiwa inadhihirisha yale G. Orwell aliyosema katika kitabu chake maarufu kinachoitwa 'the animal farm' shamba la wanyama kuwa kuna binadamu wengine ni zaidi ya wengine.
ninakuwa ninajiuliza kuwa inawezekana ni mfumo wetu wa sheria una macho ama watendaji wenye dhamana ndio wanaoangalia na kuifanya sheria kuwa na macho na kuipotezea imani yake kuwa sheria ni msumeno!
Nimemshangaa jaji mkuu amabye ameshangazwa na kitendo cha wasalama kumpitisha kigogo katika mlango unaotumiwa na mahakimu, hivi hajui kuwa watuhumiwa wengine ni mahakimu tayari, kwenda mahakamani kwao ni kama kuwazuga tu na ndiyo maana wakati wanaogoma wanarundikwa kwenye makarandinga wao wanaletwa na taksi amabyo inalindwa na polisi wenye silaha ili kutotota nafasi kwa 'washenzi' kutotoa habari kwa umma.
Najiuliza wale ndugu wa mtuhumiwa waliowafanyia uhuni wapigapicha wa habari corparation walikuwa wanajua kuwa ni lazima ndugu yao atapewa dhamana! Hivi kama hakimu angekataza dhamana nani angeshambuliwa na ndugu hawa amabo mahakama waliifanya kama sehemu ambako mwali anatolewa kwa kwenda na kanga huku walinzi wa usalama wakiwaangalia kana kwamba wanachofanya kinaruhusiwa.
Ingekuwa ni 'kapuku' kweli angeruhusiwa kwenda hata na 'leso' ikiwa tu simu ya kapuku ikiita basi hima askari atakufuata na kukugombeza huku hakimu akitishia kukuadhibu kwa kuleta kelele kortini.
Sheria haina macho lakini waliodhaminiwa na wanachi kuitunza na kuiimarisha wamekuwa wabaguzi huku vigogo wakikrimiwa na walalahoi wakinyanyaswa hata kwa kufanya mepesi dhidi ya mazito yanayofanywa na vigogo
Ni jana tu ambapo wanachuo walishuhudia timu yao ya mpira wa miguu ikicheza na timu ya vijana wa mtaani wanaojulikana kama 'nantes' timu ambayo mfadhili wake mkuu inaaminiwa ni mhasibu wa chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere ndugu Magulumengi.
Ikicheza kitimu timu ya chuo ilikukuwa ya kwanza kuliona lango la wapinzani wao kupitia kwa mfungaji wake makini Magesa aliyefunga bao tamu baada ya kupata pasi safi toka kwa kiungo mfungaji Marijani.
Bao hilo liliwafanya wageni wachanganyikiwe huku kiungo wa nantes Dinno akihangaika kuipita ngome ya chuo iliyokuwa chini ya ulinzi wa dogo Allan. Hadi kipindi cha kwanza kinakwisha chuo walikuwa wakiongoza kwa goli moja.
Kipindi cha pili timu ya wageni ilifanya mabadiliko yaliyosaidia kupatikana kwa goli la kusawazisha lililofungwa dakika 20 baada ya kipindi cha pili. Bao hili liliwaduwaza chuo na kujikuta wakicheza bila mpangilio na mabeki wakicheza faulo zilizosababisha chuo kufungwa goli la pili. faulo iliyopigwa dakika za majeruhi pembeni mwa lango la timu ya chuo ilizaa goli lililowaduwaza wachezaji na mashabiki wa chuo kwani licha ya kuwa timu yao ilifungwa bali lilimaanisha uteja wa kudumu kwani tangu 2005 timu ya chuo haijawahi kuwafunga vijana wa nantes ambao huongozwa na kapteni mwenye maneno mengi Ben Shoo.
Pamoja na mabdiliko makubwa yaliyofanywa na chuo ya kuwaingizi Chidi, Munga na seki timu ya chuo ililala na kumwacha mshabiki ambaye hujifanya kocha hanzuruni akiapa kutoshangilia tena timu ambayo haina dhamana.
Mashabiki walioongea na mwandishi wa blog hii walionekana kukerwa na kufungwa huku na wakaifananisha timu yao kama timu ya aseno ambayo mbali na kucheza mpira na kuumiliki kwa muda mrefu alkini wamejikuta hawana chao msimu huu.
Wednesday, March 14, 2007
Thursday, March 08, 2007
JAMII IWAANGALIE WANAWAKE WAJAWAZITO!!!
Nimeamua kuandika waraka huu nia kubwa ikiwa ni kutaka kukuonesha wewe msomaji adha wanayoipata wanawake wengi wa Kitanzania hasa wanapokuwa wajawazito. Wanawake wajawazito hasa wale wa vijijini wanapata wakati mgumu sana na unaoogopesha pindi wanapokuwa wakifuata huduma ya 'kujifungua' katika hospitali za serikali.
Hospitali nyingi za serikali zimekuwa si rafiki wa wajawazito hasa wale wanaotoka vijijini ambako umaskini humsabahi kila mtu katika nchi hii inayohubiri maisha bora kwa kila mtanzania. Wanapofika hospitali wanalazimika kununua mahitaji ya kupatiwa huduma ilhali serikali imetangaza kuwa 'vifaa' hivi hupatikana bure kwa wote, hii si kweli.
Wanahitajika kujinunulia vifaa hivi ambavyo kwao ni ghali sana na wengine huamua kabisa kuacha kwenda hospitali kwani masaibu watakayokutana nayo huko yanatisha.
Kuna baadhi ya hospitali, tena nyingine zipo mijini kabisa kina mama wajawazito wamekuwa wakirundikwa wodini kama magunia ya viazi, huku kitanda kimoja kikilaliwa na wajawazito wawili 'wenye bahati' na wasiona bahati basi wasubiri saa katika sakafu.
Ni serikali yenye jukumu la kuhakikisha kuwa hospitali zake zina si huduma bora na vifaa tu bali wahudumu wapo wa kutosha na wanaowezestoa huduma kwa kila mmoja bila kujali hali ya kipato chake.
Leo tunapoungana na wanawake kushehereke siku yao duniani ni jukumu la kila mwanajamii na serikali kujiuliza wanawake wajawazito wanasaidiwa vipi
Mama, mwanao nakuandikia waraka huu mfupi kwa ajili ya kukupongeza na kukushukuru kwa yote uliyofanya na unaendelea kuyafanya nia kubwa ikiwa ni kuhakikisha kuwa mwanao ninakuwa 'huru'. Mama, leo unaungana na wanawake wengi duniani kusheherekea siku hii nzuri na inayoheshimiwa na kila mwanadamu. Nakupongeza mama yangu kwa kuwa makini katika kuhakikisha ninakuwa na ustawi ulio mzuri na wenye maisha mazuri.
Nina mengi ya kukuandikia kuonyesha furaha yangu wakati unaungana na wenzako katika siku hii muhimu, sitaki nikuchoshe ila tu tambua ya kuwa u mwanamke bora zaidi na unastahili yote jamii inayoweza kutoa kwa ajili ya ustawi wako ambao unamaanisha ustawi wa jamii nzima.
Hongera mama
Wanawake duniani kote leo tarehe 8mwezi wa 3 wanaungana wote duniani kutambua siku yao. Jamii nyingi duniani zinawachukulia wanawake kama binadamu wa 'pili' huku wanaume wakiwa ni wa kwanza bila kujali mchango mkubwa unaoletwa na wanawake katika suala zima la kuleta maendeleo kwa taifa na familia kwa ujumla.
wanawake ni muhimu sana kwa taifa kwani ukiachana na jukumu lao kubwa la kuongeza 'wanachama' katika taifa, wamekuwa ni mstari wa mbela katika kujenga jamii bora kabisa kwa kujenga misingi imara ya tabia za watoto na hivyo kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo ya jamii.
Jamii zetu kwa sasa zimebadilika sana katika suala la kumtambua na kumthamini mwanamke, hapo zamani mwanamke alikuwa anabaguliwa na familia katika suala zima la elimu lakini kwa sasa hali ni tofauti kwa uwezo wao mkubwa darasani na mawazo yao endelevu vimechangia kujenga misingi madhubuti katika nyanja ya elimu. Kwa nchi kama tanzania, wasichana miaka miwili mfululizo wamekuwa wakiongoza katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne na sita. Hii imeongeza changamoto kwa jamii kuona kuwa mtoto wa kike anafaa sana kusomeshwa na kama ule usemi wa msomi maarufu unaosema 'kumwelimisha mwanamke ni kuelimisha jamii' unatimia
Wednesday, March 07, 2007
Ni majuzi tu rais wetu mpendwa na ambaye pia ni mwenyekiti wa chama chetu kinachodumu amerejea kutoka safari ambazo sasa zimekuwa ni za kawaida kwake. Inawezekana watu wanaolaum safari hizi hawajui kuwa huyu aliwahi kuwa waziri wa mambo ya nje! Wewe unaonaje, unadhani hajasahau kuwa cheo sasa ni kipya?
Msomaji wa machweo, nimekuwa nikikuandikia kuhusu mabadiliko makubwa yanayoendelea hapa chuoni ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya jina la chuo cha kumbukumbu ya nyerere mpaka kuteuliwa kwa viongozi wa kuongoza chuo na kubwa zaidi maktaba ya kompyuta kuanza kutumika.
Kwa mabadiliko haya, nami pamoja na waandaaji wa blog hii tunajipanga ili kuiboresha blog hii ivutie na pia kuongeza 'utamu' kwako msomaji.
Kwa sasa unapofungua blog pembeni utaona viunganishi ambapo utaweza kutembelea blog nyingine za kiswahili ikiwemo ya Ndesanjo, Mkina, Ngurumo na ile ya katuni za Kipanya.
Mengi yanakuja nami nawaahidi kuwapa kile mnachoona kinafaa, tafadhari msisite kutuma maoni yenu katika blog hii
Friday, March 02, 2007
Leo imekuwa ni siku njema na ya furaha sana kwa walioteuliwa kushika nyadhifa hapa chuoni, kama huna habari ya uteuzi huu ngoja nikupashe kidogo. Juma lililopita bodi ya chuo chini ya m/kiti dr Salim A. Salim iliwateua ndugu Mushi na ndugu Luambano kushika nyadhifa za juu kabisa hapa chuoni, Mushi aliteuliwa kuwa naibu wa mkuu wa chuo na Luambano kuwa msajiri wa chuo, hii imekuwa ni habari njema kwao.
Licha ya uteuzi kumaanisha 'posho' kuongezeka na majukumu tele lakini uteuzi huo umeendana na kuletwa kwa 'mashangingi' magari mazuri ya kifahari (sema ya anasa) ili kurahisisha utendaji kazi wa vionngozi hawa.
Jumuia tumeombwa kutoa ushirikiano kwao lakini hatujaona sehemu wao walipoombwa kutoa ushirikiano kwetu, labda tutapata lifti! Tusubiri tuone
Niliwahi kukuandikeni kuhusu kutokuwapo kwa huduma ya kisasa ya intanet hapa katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere, kwa sasa hii leo inaweza kuwa ni historia kwani kwa muda huu ninapokuandikia nimo ndani ya chumba ambacho zamani kilikuwa kimefungwa kwa makufuri makubwa ya solex na milango ya vyuma yakihifadhi kompyuta, ninakuandikia habari hii huku mwalimu wa somo akiwa pembeni.
Wanachuo sasa hatuna haja kwenda 'ferry' ili kupata huduma hii muhimu ambayo baadhi ya 'watu' wanaiona kama ni ya anasa.
lakini kikubwa kinachoonekana hapa ni ratiba ya kuingia madarasani kwani kuna baadhi ya wanafunzi wanaamua kushinda 'lab' wakiamini mtandao ndo kila kitu, labda ni 'ugeni'.
Tusubiri tuone mabadiliko ambayo yameendana kabisa na uongozi mpya wa chuo
Friday, February 16, 2007
Wiki jana nilikuwa ndani ya basi toka Dar kuelekea Mwanza kwa ajili ya kukamilisha utafiti wangu kuhusu kuongezeka kwa wapigadebe katika vituo vya mabasi. Chuo kilitoa muda mfupi uliolazimu sisi tunaotoka mikoani kutafuta usafiri wa haraka ili kuwahi kalenda. najua unafikiria ndege, kwangu mimi usafiri wa haraka si ndege, ni basi.
Tuliondoka kwa basi la Mohammed ambalo nalo kama ilivyokuwa kwa barabara ya kati toka dodoma kwenda singida, lilikuwa ni bovu isivyo kawaida kiasi cha kutulazimu kuingia Dodoma saa 4 usiku. hata hivyo hii si ishu yangu ya leo, leo nataka kuongelea ubovu wa barabara hii maarufu kama njia ya kati.
Barabara hii ni mbovu sana na hasa katika kipindi hiki cha mvua, maeneo ya manyoni na baadhi ya vipande vya tinde hali ni mbovu sana.
Hali hii inashangaza sana kwani serikali kuanzia ile ya awamu ya tatu ilikuwa ikihubiri kwamba ni mapema tu mtu ataweza kutoka mwanza mpaka mtwara kwa gari dogo 'tax'.
Kandarasi aliyepewa kufanya shughuli ya kujenga barabara hii angekuwa ni mtanzania basi tungesema ni ndugu wa kigogo lakini kwa kuwa ni mgeni basi hapo kwa akili ya kawaida kabisa tuliyozoea sis basi tunasema kuna mtu kala, kwani huwezi kumpa mkandarasi asiye na uwezo kazi kubwa kama hii.
Nitakuandikia tena kuhusu tatizo la usafiri ambalo kwa kuwa viongozi wanatumia usafiri wa haraka,ndege, kwao si tatizo
Thursday, February 01, 2007
Unashangaa kuona kichwa hicho, najua unategemea kabisa hili kutokuwa tatizo katika chuo tena cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere. Umekosea.
wakati shule zinazoitwa za 'academy' (sio academy ya mwalimu nyerere) siku hizi watoto wanafundishwa kompyuta, hali hii ni tatizo hapa chuoni kwani ukitaka kufahamu ni wanachuo wangapi wana uwezo wa kutumia kompyuta basi idadi yao itakusikitisha na kukufanya labda ufikiri kuwa hapa kumejaa ubabaishaji tu.
Sio kwamba kompyuta hakuna, la, zipo kama 40 lakini zima ndani ya vyumba vyenye milango ya chuma na mlinzi nje kuhakikisha kuwa hakuna anayechungulia na kuona vitu vya ajabu, kompyuta.
Mkuu kateuliwa na labda tunaweza kuanza kuiona kompyuta 'live'
Tungoje na kwa wale wasiojua basi wasubiri au waende wakajiandikishe katika akademia za kitoto
Kila mmoja alikuwa na mshawasha wa kutaka kujua ni nani atashika nafasi ya ukuu wa chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, wengi walikuwa wakifikiria mabadiliko......
Majuzi waziri wa elimu ya juu kafanya kile ambacho alipaswa akifanye, kuteua mkuu wa chuo nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na daktari Magotti ambaye pia ni kada mkubwa chama tawala CCM.
Uteuzi umefanyika na aliyeteuliwa kuwa mkuu wa chuo ni yuleyule aliyekuwa akikaimu na ambaye amekuwa mkuu wa chuo tangu kilipokuwa chuo cha chama na sasa chini ya serikali.
Ndiyo, jina jipya la chuo lakini mkuu yuleyule, hii ina maanisha kuwa tutegemee mengi na makubwa toka kwa kiongozi mkongwe.
machweo inamtakia dr Magotti kazi njema na itampa ushirikiano wa kutosha kama tulivyoombwa na msarifu ambaye naye ana kaimu nafasi hii, kwa maoni yetu sisi wana machweo tunadhani hata msarifu arudishwe yuleyule na pia korando likarabatiwe liwe jipya.
Thursday, December 28, 2006
Naaam, rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania JMK ametimiza mwaka mmoja tangu watanzania wamuamini katika kuwaongoza.
Mwaka mmoja si kipindi kizuri cha kuamua na kutoa tathmini ya kilichofanya na mtu tunayetegemea atuongoze kwa miaka mitano.
Waandishi wengi sana wamejitokeza kutoa na kuelezea mafaniko ya rais ndani ya mwaka huu mmoja, kila mmoja amemsifu na hii ni haki yake.
Tunajua kabisa rais amekuwa ni kipenzi cha waandishi wengi tangu enzi za mchakato wa uchaguzi na mpaka anakuwa rais, kwa hali hii si rahisi kwa watu waliokuwa wakimtukuza kama mtu mwajibikaji kuanza kumtenga na kueleza uhalisia.
Kwa upande wangu mimi sioni mafanikio yoyote kama baadhi ya waandishi wanavyotaka kutuaminisha na vyombo vyao, tazama hali ya usafiri kwa wakazi wa Kigamboni jirani kabisa na ikulu, siwezi kuyaona mafanikio ya kodi tunazoambiwa zinakusanywa kwa mabilioni wakati hakuna pantoni la uhakika, au hawa waandishi wanataka tufe baharini na waandike habari za kiongozi kuja kuwatembela ndugu zetu.
Hizi sifa anazopea JMK ziangaliwe tena kwani hakuna mabadiliko yoyote
Saturday, December 23, 2006
Juzi tumekuwa na kikao na mshauri wa wanafunzi (mwaka wa pili) kikao kilikuwa na mabo mengi yaliyoongelewa kikubwa ikiwa ni masuala mbalimbali ambayo wanachuo tunaona hayaeleki kwa kuwa hayajawekwa wazi na uongozi, kwa mfano suala la ada pamoja na utafiti , inakuwaje tunatoa pesa nyingi kila mwaka wakati utafiti tunaufanya kwa mwaka mmoja tu, pia tunalipa kodi kubwa ya pango (21000/=)kila mwezi ilhali huduma katika hosteli ni mbovu hususani ubovu wa makabati na upungufu wa matundu ya vyoo, hebuchukulia mfanowa hosteli ya Kizota juu ambayo inawakaazi karibu 70 lakini wote hawa wanategemea matundu mawili ya vyoo pamoja na milango minne ya mabafu!
Huduma ya chakula inatolewa na mtu mmoja tu, kwanini, ina maana hakuna watu wengine wa kutoa huduma kwa wanafunzi hasa ukizingatia kuwa mtoa huduma huyu hatoi huduma zinazoendana na namba ya wanachuo! Nani katika menejimenti anamlinda,kwanini serikaliya wanafunzi inasema kuhusu tatizo hili na blahblah toka kwa utawala ndo zinatawala!
Usiogope! haya yalijibiwa na mshauri ambaye kwa kweli alijitahidi sana kupunguza jazba za washikadau!
Hii ndo hali halisi iliyopo hapa chuoni na labda tutegemee mabadiliko kwani ukarabati uliochukua muda mrefu kuliko ujenzi ndo kwanza upo katika hatua za mwisho huku sisi wanachuo tukikosa maktaba na hivyo kufanya masomo yetu kuwa magumu hasa ukizingatia kuwa kutegemea maktaba za nje ni ghali kwa mabo ya kivuko ambacho kinachukua muda mrefu kuvusha watu huku ratiba ikiwa inatukaba kwa sana. Hii yote tisa ni hili lililotokea mkutanoni lilianza hivi...
baada ya dean kutoa nafasi kwa wanachuo kuuliza maswali na kutoa yote yanayowakereketa, akasimama mwanadada wa kozi ya Gender anaitwa dada Agnes, huyu ni mlemavu wa macho, haoni na kwa hapa chuoni yupo peke yake.
Aliposimama kuongea kila mtu ukumbini alinyamaza ili kusikiliza nini anasema, akiongea kwa sauti inayosikika masikioni kwa uzuri kabisa aliyatoa yake mengi na hasa lile ambalo yeye analiona kwamba kuwepo kwake hapa chuoni kumekuwa ni mzigo na inawezekana kwa kuwa chuo kimemuona ni mzigo kimeshindwa kuwapa nafasi walemavu kama yeye walioomba nafasi za masomo chuoni.
Yeye anakabiliwa na matatizo mengi katika kujisomea kwani gharama zote zinamwangukia yeye na chuo kinashindwa kumsaidia japo kwa kumtafutia karatasi za kuandikia. Alijaribu kuwapatia management anuani za mashirika ambayo yanawasaidia watu wenye matatizo kama yake lakini anashangaa hakuna chochote kilichoendelea, hajapata msaada.
Wote tulinyamaza na sikia jibu hili toka kwa Dean "si kweli kwamba chuo kinakuona wewe kama mzigo, kinajivunia kuwa nawe hapa na hata huwa naona wageni wanapotutembelea hapa huelezwa kuwepo kwako hapa". Naam, tulishukuru kwamba mshauri mwenyewe aliahidi kumsaidia dada huyu ili aweze kufanikisha kile kilichomleta hapa na kumwelewesha kwamba chuo hakina noma na kuwepo kwake hasa ukizingatia vyuo vyenyewe ndo hivi tu.
Kikao hakijaisha, nitakuwa nikikutaarifu kadri siku zinavyokuja kwani kuna fukuto ambalo linahitaji majibu na kwa hulka ya 'wakubwa' labda wanasubiri kitendo kitokee ndipo waseme wanavyoona ni sahihi kwa wanachuo kufanya
Naam, sherehe za kuadhimisha miaka 45 ya uhuru wa Tanzania (ipi ilipata uhuru, Tanganyika au Tanzania!) zimemalizika na kamati imevunjwa huku waziri mkuu akijipanga tena kuongea na wafanyabiashara ili wasaidie katika maandalizi ya sherehe zijazo.
Sherehe hizi zimefanyika kama kumbukumbu kuadhimisha uhuru wan chi yetu toka kwa wakoloni, waingereza ambao walipewa jukumu la kuwa waangalizi (Tanganyika became the british protectorate) wan chi yetu kwani Un haikuwa watawala na mnamo tarehe 9desemba 1961 bendera ya malkia ikashushwa na bendera yenye rangi nne kumaanisha Tanzania ikapandishwa.
Miaka 45 si mingi sanakwa miaka uhai wa taifa japo si haba kujivunia miaka hii tukiwa huru, na kwa kufikisha miaka hii hakuna haja ya kuacha kusheherekea kwa mbwembwe na majivuno mengi kuonesha ni nini maana ya kuwa huru.
Kusheherekea uhuru ni jambo muhimu sana yaani ni kama mtu wa kawaida anaadhimisha ‘birtday’ yake. Uhuru unamaanisha hali na uwezo wa kujiamulia mabo yako bila kuingiliwa na nchi au taifa jingine (sovereignity).
Sherehe za mwaka huu zimekuwa tofauti kidogo na zile zilizokuwa zikifanywa na wamu zilizopita. Hizi zilikuwa ni za ari mpya, nguvu mpya na ari mpya.
Zimekuwa ni tofauti kwa maana ya kwamba hizi zimeendana na mkesha wa nguvu uliooneshwa moja kwa moja na luninga ya taifa (TVT). Hii iliwapa nafasi watanzania wote kushuhudia sherhe hizi zilizoambatana na tatizo la kukatika katika kwa umeme..
Suala la kukatika kwa umeme siyo ishu iliyonishawishi na kunivuta kuandika kuhusu maadhimisho haya. Na wala sitaongelea suala la waziri mkuu kuwaomba wafanyabiashara wakubwa wajitokeze kuchangia na kufanikisha sherehe hizi zinazokadiliwa kugharimu bilioni moja na ushee pesa za kitanzania.
Wengi wameongelea kuhusu sherhe hizi, wapo waliohoji kuhusu suala la ni nchi gani iliyopata uhuru, mwandishi nizar visram yeye anashangazwa na tukio la waziri mkuu kukutana na wafanyabiashara ili wafanikishe sherehe hizi, kwake hili ni kama kuibinafsisha siku muhimu kwa watanzania wote.
Wanasosolojia nao hawakuwa kimya katika kuadhimisha shehere hizi zilizoshuhudia kwa mara ya kwanza madege yetu ya kivita yakipita kwa mbwembwe kusherehekea siku hii muhimu, wao wamehoji kuhusu ni nani hasa anayesheherekea siku hii kwa watanzania. Kwao matabaka yanayojitokeza nchini yanawafanya wahoji je ni kweli sherehe hizi ni za wote au ni kwa baadhi ya watanzania? Haya yameongelewa na si vibaya kuyajadili katika nchi hii inayoadhimisha miaka 45 ya uhuruhuju pengo kati ya maskini likiwa linaonekana wazi, maendeleo ya mijini na vijijini yakiwa na tofauti kubwa na huku mipango ya maendeleo vijijini ikijadiliwa na watu wa mjini.
Sasa turudi kwenye mada kwani isije nikaonekana nataka tu kujaza kurasa, lakini hata hayo niliyoyagusa ni muhimu yakajadiliwa na pia yatatuongoza katika kutambua mada ya leo.
Mavazi ni kitambulisho kikubwa cha uataifa wa mtu kama zilivyo pesa, wimbo wa taifa pamoja na ramani ya nchi. Leo hii ukiangalia nchi huru nyingine za kiafrika utaweza kuwatambua raia wan chi hizi kwa kuyaangalia mavazi wanayovaa, hebu chukua mfano wan chi za Nigeria, Ghana na afrika kusini. Tanzania na uhuru wetu bado hatuna vazi letu la taifa.
Katika mkesha wa kukaribisha saa sita,pale mnazi mmoja, wote tutakuwa mashahidi kwa namna viongozi wetu walivyokuwa wamependeza katika mavazi mazuri ya gharama toka magharibi. Kwa kifupi mavazi hasa yaliyokuwa yamevaliwa na viongozi yalikuwa ni kama tunaadhimisha uhuru wa nchi moja ya kimagharibi.
Tumeshuhudia umati wa watanzania waliohudhuria mkesha huu wakiwa na mavazi ya aina tofauti, huku wengi wasio jukwaani wakiwa ndani ya mavazi yaliyo kwenye ‘chati’ kwa sasa miongoni mwa watu wa chini ‘mitumba’.
Huku mkesha ukiambatana na ulipuaji wa baruti, tumeshuhudia viongozi wetu waliokuwa wakishuka toka katika magari makubwa nay a gharama wakiwa ndani ya suti nzito na za gharama. Tumeshudia viongozi wanaume wakiwa ndani ya suti nzito toka kwa wabunifu wa kimagharibi, mavazi ambayo yanaonesha kabisa kwamba inawezekana tukawa tunajitawala kwa kufikiri na kuvaa kimagharibi! Angalau mavazi yaliyokuwa yamevaliwa na wanawake viongozi yalijaribu kuonesha utamaduni wa kiafrika kwa kuuvaa Unaijeria na Ughana.
Kwa maisha ya leo yawezekana kabisa baadhi ya watu wakaona suala la mavazi ni ishu ndogo sana kiasi cha kujadiliwa katika kuadhimisha miaka 45 ya uhuru wan chi yetu. Kwangu hili ni suala la kujadili kwani kujitawala ni pamoja na kuonesha waliotutawala kwamba sasa sisi tuko huru yaani tunaweza hata kuwa na maamuzi katika mavazi ya kuvaa.
Uhuru una maana nyingi sana ikiwa ni pamoja na kuonesha hali ya kuwa na maamuzi katika utamaduni wako unaoongoza maisha yako ya kila siku. Mavazi ni sehemu ya utamaduni.
Utamaduni ni zaidi ya ngoma tunazozishudia zikialikwa kutumbuiza katika sherehe hizi. Ngoma kwa sasa kwa baadhi ya watu zimekuwa zikionesha ukale, kinachotamba sasa ni utamaduni wa ‘bongo fleva’. Tumeshuhudia kila mara vikundi vya ngoma vilipokuwa jukwaani havikupata mapokezi mazuri toka kwa hadhira lakini pale walipopanda ‘wanaume tmk’ wakiwa wamevaa mavazi ya kisasa kelele za kushangilia zililipuka. Huu ndio utamaduni tunaoushabikia sasa na miaka 45 ya uhuru.
Mwandishi mahiri katika suala la utamaduni wa mwafrika, mwanazuoni Kihumbi Thairu (the African Civilization) anawashangaa wale wote wanaodharau mavazi yetu na kukumbatia mavazi ya kigeni yasyojali hali ya hewa na mazingira ya nchi zetu za kiafrika. Mavazi haya ya kigeni tunayoyavaa sit u kwamba yanashindwa kututambulisha sisi ni kina nani bali yanatufanya tukose sababu ya kusheherekea uhuru wan chi yetu.
Kwa jinsi kila kitu kilivyokuwa kikifanyika pale mnazi mmoja huku kila mmoja akiwa katika vazi lake ni uthibitisho tosha kwamba kwa sasa tuko huru kweli kweli na mwingereza hana chake tena..
Jukwaa zima lilikuwa limetawaliwa na mavazi ambayo hayakuonesha maana ya kusheherekea uhuru wetu. Miaka 45 ya kujitawala ni mingi sana kuweza kujiamulia ni nini tunapenda kuvaa, baadhi yetutumechagua kuuvaa umagharibi ndani ya umaskini wa uhuru.
Natambua juhudi zilizofanywa na baadhi ya watu waliokuwa na mapenzi ya kutupatia watanzania kitambulisho kwa kubuni vazi la taifa. Hii ilikuwa nikipindi cha miaka ya 2000 na ninakumbuka kwamba baadhi ya wabunifu walifika mpaka kule Dodoma nyumbani kwa bunge la watanzania.
Kama ilivyo kawaida ya waswahili ‘watu wa ahadi’ suala hili sasa hakuna anayeliongelea na hata vazi lililoshinda nadhani sasa litakuwa limepambwa makumbusho kwa ajili ya kuvionesha vizazi vjavyo kwamba hili ni vazi la kitanzania ambalo halikuwavaliwa kwani wazazi wao walikuwa wakivaa mavazi mengine kwa kuwa tu walikuwa huru, wenye uwezo wa kujiamlia mabo yao wenyewe bila kuongozwa na mtu mwingine.
Kwangu mimi tofauti niliyoiona katika upande wa mavazi ina maanisha vitu vingi sana ikiwemo suala la kuibuka kwa matabaka katika jamii yetu. Matabaka ambayo yanashindwa kuelewa maana ya uhuru wa nchi yetu.
Mika hii 45 ya uhuru na mavazi yaliyovaliwa na wakati wa sherehe hizi na hasa yale ya viongozi wetu yanaonesha kabisa kuwa sasa uhuru wetu umekuwa ni kwa ajili ya kuchangisha pesa toka kwa wafanyabiashara wakubwa ili kufanikisha sherehe hizi ambapo mtanzania wa kawaida anaishia kukesha akiwa amevaa mavazi yasiyoeleka hasa mitumba huku viongozi wakijichana wakiwa ndani ya suti nzito zilizobuniwa na wabunifu toka kwa wale tuliokuwatukiwaita wakoloni na mabeberu.
Kwa kuona kwamba katika sherehe hizi hakuna aliyekuwa uchi, basi sula la vazi la taifa si muhimu hasa ukizingatia kuwa nchi yetu na utawala huu una mambo mengi ya kuonesha sasa tuko huru. Kila mmoja amevaa nguo anayoitaka na kumudu kununua kutokana na ruhusa ya kipato chake. Kwa kuwa na mambo mengi ya kuleta maisha bora kwa kila mtanzania suala la mavazi si la kujadili kwa sasa
Ni kipindi kingine tena msomaji wa blog hii ambapo wakristo wote wanaungana na wenzao wengi duniani katika kusheherekea sherehe 'birthday' ya mkombozi wa maisha yao Bwana yesu Kristo. Hii ni siku kubwa na inatukumbusha juu ya nafasi yetu tuliyonayo katika kutekeleza lile lililotuleta duniani na tunahitajika tufanye nini ili tuingie mbinguni(kwa wanaoamini katika hili tu-wakristo)
Machweo inapenda kuwatakia watu wote msimu mzuri wa sikukuuza 2006 pamoja na Heri ya mwaka mpya 2007
Monday, December 18, 2006
CHUO KIKUU BILA MAKTABA!
Ukarabati umechukua miezi minne na sehemu na mpaka sasa hakuna kilichokabidhiwa kwa chuo ila jengo linang'aa kwa rangi nyeupe
Mmeyasikia wenyewe, hakuna haja ya kuyarudia kuyaandika malumbano yanyoendelea kati ya shirika la ugavi la tanesco na 'wasanii' wanaojiita richmond. Hawa waliingia mkataba wa kuzalisha megawati 100 za umeme kwa kutumia majenereta yao waliyotoa marikani na kuiuzia tanesko. mitambo iliwasili na baada ya mbwembe nyingi sana za kuahidi kuzalisha kwanza megawati 20 kabla ya tarehe 1desemba2006 huku wakisaidiwa na waziri wa nishati, hakuna umeme uliozalishwa.
Sasa wamekuja na longolongo ya kusema kwamba eti tanesco imewapatia gesi chafu yenye kokoto! ukiniambia gesi kuwa na kokoto kwangu mimi nitakushangaa, hivi kumbe gesi ina kokoto kama zile za kujengea zege!
bado ninalia na wale wote waliofunga mkataba na kampuni hili linalodai lina makazi yake marekani huku mwakilishi wake hapa akiwa na mkoba tu, huu ni usanii
Hivi JK anasubiri nini kuwawajibisha wanasiasa waliosani mkataba huu, wakati mwingine ninajiuliza kama waziri mkuu alikuwa na sababu ya kulijibu shairi la bwana Marwa akijitapa kuwaonesha viongozi waadilifu waliojaa tele hapa nchini, yaani wamejaa tele halafu wafunge mikataba mibovu kama hii na bado waendelee kuwa wasafi na waliojaa tele.
Jeshi la polisi lipewe kazi ya kuwasaka wote 'waliojaa tele' na kusaini mkataba huu ili wafikishwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake! (unakumbuka enzi za kufilisiwa)
majambazi yakikamatwa basi tv zitarusha sana ama kibaka akiwa mikononi mwa wanachi wenye hasira, kila mmoja hunyanyua mkono ili amwadhibu kibaka lakini majambazi ya peni hapa kwetu yana heshimika sana na wanaonekana mahujaa, naamini kabisa richmond wamekula na 'waliojaa tele' na wanaendelea kutanua katika magari yenye viyoyozi kwani tarehe za pcb ni nyingi kurekebisha na kuua so.
Kaeni kimya mkisubiri uongo mwingine toka kwa wasanii wa Richmond
Monday, December 04, 2006
Usiogope. Nadhani unakumbuka enzi za akina chifu Mangungo wa msovero na lile jasusi la kijerumani Karl Peters, enzi hizo watawala wetu walilazimishwa na kulazimika kusaini mikataba feki iliyowafanya wapoteze tawala zao katika nchi walizokuwa wanazitawala.
Kuna sababu nyingi zilizowanya wasaini mikataba hii, moja kubwa ikiwa ni ile hali ya kujua kusoma na kuandika lugha za kigeni. pamoja na kusaini mikataba hii feki watawala hawa wa kiafrika walikuwa wakichukua muda kuijadili na kuifikiri mikiataba hii.
Tofauti na sasa ambapo watu tuliowaamini katika kuongoza nchi yetu tajiri yenye watu wapole na wakarimu, ndio wanaotuumiza na kutufanya tukae gizani kwa kuingia mikataba ya kutunyanyasa huku wao wakifaidi 'aksante' waliyopewa na mambazi haya.
Fikiria mikataba yote ambayo serikali yetu imesaini, fikiria ile ya madini, IPTL na sasa huu mpya wa sijui inaitwa Richmond, hivi mikataba hii inamsaidia nini mtanzania wa kawaida. Ninasema wa kawaida kwa sababu sasa watanzania tunatofautiana, tuna matabaka yaani ni kama nchi za kibepali.
Mikataba hii walioisaini wapo, tunawajua na wanaendelea kula kuku tu na huku wakituimbia nyimbo za kutukaririsha ya kuwa uchumi wetu unakua! unakua au unakuwa!
Mimi si mchumi lakini siamini ukuaji wa uchumi huku nchi ikiwa haina umeme wa uhakika, ni mgao tu kwa kwenda mbele huku wale tuliowaamini kutuwakilisha bungeni wanakaa kimya na kujadili mambo hata yenye jibu tayari, wanajadili eti kuhusu vazi la spika, inamaana spika yuko uchi au wanadhani wakimnunulia spika vazi jipya ndipo watajadili hoja tunazotaka wazijadiliili.
Kwanza hilojoho akilifua atalinyoosha na nini? OOOps nilisahau kumbe wao ni tofauti na mimi, wao kila siku ni full kipupwe, full kiyoyozii
Usiogope. Nadhani unakumbuka enzi za akina chifu Mangungo wa msovero na lile jasusi la kijerumani Karl Peters, enzi hizo watawala wetu walilazimishwa na kulazimika kusaini mikataba feki iliyowafanya wapoteze tawala zao katika nchi walizokuwa wanazitawala.
Kuna sababu nyingi zilizowanya wasaini mikataba hii, moja kubwa ikiwa ni ile hali ya kujua kusoma na kuandika lugha za kigeni. pamoja na kusaini mikataba hii feki watawala hawa wa kiafrika walikuwa wakichukua muda kuijadili na kuifikiri mikiataba hii.
Tofauti na sasa ambapo watu tuliowaamini katika kuongoza nchi yetu tajiri yenye watu wapole na wakarimu, ndio wanaotuumiza na kutufanya tukae gizani kwa kuingia mikataba ya kutunyanyasa huku wao wakifaidi 'aksante' waliyopewa na mambazi haya.
Fikiria mikataba yote ambayo serikali yetu imesaini, fikiria ile ya madini, IPTL na sasa huu mpya wa sijui inaitwa Richmond, hivi mikataba hii inamsaidia nini mtanzania wa kawaida. Ninasema wa kawaida kwa sababu sasa watanzania tunatofautiana, tuna matabaka yaani ni kama nchi za kibepali.
Mikataba hii walioisaini wapo, tunawajua na wanaendelea kula kuku tu na huku wakituimbia nyimbo za kutukaririsha ya kuwa uchumi wetu unakua! unakua au unakuwa!
Mimi si mchumi lakini siamini ukuaji wa uchumi huku nchi ikiwa haina umeme wa uhakika, ni mgao tu kwa kwenda mbele huku wale tuliowaamini kutuwakilisha bungeni wanakaa kimya na kujadili mambo hata yenye jibu tayari, wanajadili eti kuhusu vazi la spika, inamaana spika yuko uchi au wanadhani wakimnunulia spika vazi jipya ndipo watajadili hoja tunazotaka wazijadiliili.
Kwanza hilojoho akilifua atalinyoosha na nini? OOOps nilisahau kumbe wao ni tofauti na mimi, wao kila siku ni full kipupwe, full kiyoyozii
Monday, November 20, 2006
MIONGONI mwa falsafa ambazo zinanigusa mno nafsi yangu ni msimamo wa Rais Jakaya Kikwete kuhusu suala zima la ukuaji wa uchumi.
Rais Kikwete amekuwa akisisitiza kuwa ukuaji wa uchumi unaoelezwa kwa wananchi na ama wataalamu wa uchumi au viongozi wa siasa, kwamba uchumi umekua huku hali za wananchi zikiwa duni haiwezi kuwasaidia.
Kiongozi huyo wa nchi ambaye nyota yake ya kukubalika inazidi kung’ara kwa rika zote na kwa watu wa kada mbalimbali, ana maana kuwa takwimu zilizoko katika karatasi zikionyesha kukua kwa uchumi ni ‘hesabu’ ambazo hazieleweki kamwe kwa mwenye njaa.
Idadi kubwa ya Watanzania ni watu masikini ambao hawawezi hata kuhimili idadi ya kawaida ya mlo wao kwa siku moja.
Ukweli ni kwamba Watanzania wengi hawana njia za kuwahakikishia wanapata chakula cha kutosha na chenye ukamili wake kwa ajili ya mahitaji ya mwili. Mwili huhitaji vyakula vya kujenga, kulinda na ‘kuunakshi’ ili uvutie.
Kutokuwepo kwa ‘msosi’ wao wa uhakika kunasababishwa na mambo mengi, makubwa yakiwa ni rushwa, kutotendewa haki, ubadhirifu wa baadhi ya watendaji wa umma na hujuma za kila aina zinazofanywa ili kuwanufaisha wachache katika jamii.
Juhudi za Rais Kikwete kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anafaidi keki ya rasilimali zetu na uhuru uliopatikana kwa ‘mbinde’ zinaonekana na dhamira yake iko wazi.
Ni dhamira hiyo inayowapa moyo zaidi wa kuwepo kwa neema kwa kila mmoja wetu, ingawa bado ipo kazi ambayo inahitaji pia ushirikishwaji wa wananchi wenyewe katika kuupiga vita umasikini, ambao ulionekana kuwa chanda na pete miaka mingi iliyopita baada ya 1986.
Hata hivyo, upo mwanya ambao hakuna anauyeuzungumzia kuwa ni kikwazo katika kuwakomboa Watanzania na ‘njaa’ inayowakabili.
Njaa ninayoizungumzia hapa ni pamoja ukosefu wa makazi bora, kuzungukwa na magonjwa kibao ya kuambukiza na zaidi sana njaa ya tumbo, ambayo kimsingi ndiyo ufunguo unaozungumzwa na Rais Kikwete.
Mwanya huo ni kuwepo kwa ‘njia nyeupe’ kwa baadhi ya wafanyabiashara kupeleka fedha za kigeni nje ya mipaka ya nchi yetu bila kuulizwa na yeyote.
Hivi sasa kila mfanyabiashara wa fedha; awe Mtanzania wa kuzaliwa, kuomba au hata kudanganya, anao uwezo wa kusafirisha kiasi chochote cha fedha bila kupitia Benki Kuu au katika taasisi zinazoshughulika na masuala ya uchumi.
Haihitaji kuwa na karatasi kutoka chuo chochote kutambua kuwepo hilo na kuthibitishwa na jinsi dola ya Marekani, paundi ya Uingereza inavyopanda kila uchao dhidi ya fedha yetu, ambayo baadhi ya watu wasiokuwa na utaifa wanaziita za madafu. Sina uhakika wanayaangua wapi hayo madafu!
Kuondoka kwa kiasi kikubwa cha fedha ndiko kunasababisha mfumuko wa bei kwa kiasi kikubwa huku wahusika wakifaidi na ‘walalahoi’ ambao ndiyo wanunuzi wakubwa wakikamuliwa hadi tone la mwisho.
Hivi sasa dola moja ya Marekani ni sawa na sh. 1,335 na kwamba kesho au Jumamosi kiasi hicho kitakuwa kimeongezeka kwa asilimia 10 au zaidi. Inatisha sana hali hii.
Nguvu ya soko la dunia mara zote imekuwa ikipimwa kwa kuzingatia fedha ya Marekani, hivyo shilingi yetu zinapokuwa nyingi zaidi kwa dola moja, uchumi wetu unashuka kwa njia moja hata kama itaelezwa kinyume chake.
Zipo nchi ambapo kupata dola moja ya Marekani lazima muhusika atembee kweli kweli kutoka Benki Kuu hadi taasisi zinazohusika, ambako atapatiwa karatasi lukuki kumuhalalisha kuwa anapaswa kupata na kutumia fedha hizo.
Lakini hapa kwetu kila kitu ni bwerere…na ruksa. Ukitaka dola za Marekani nenda tu mtaa wowote, hata kama ni dampo kule Tabata, utapata tu. Hakuna haja ya kuuliza benki ziko wapi. Kwa nini ujisumbue bwana! Ya nini! Ndivyo tulivyo.
Inaweza kabisa kuelezwa kwamba KONA YANGU inahitaji kuwepo kwa urasimu uliokuwepo miaka mingi iliyopita. Hapana hiyo siyo nia yangu.
Lakini ieleweke kuwa bila udhibiti wa fedha hizo za kigeni tutakuwa tukitwanga maji kwenye kinu, na kwamba kauli za viongozi wetu zinaweza kuwa zile zile zilizozoeleka masikioni mwetu.
Hakuna maendeleo bila udhibiti wa mambo kadha wa kadha ikiwemo rushwa na dhambi nyingine, ambazo nimekuwa nikizipigia kelele kila ninapopata nafasi ndogo katika ukurasa huu kueleza.
Ni vyema sasa serikali yetu ikabuni mbinu za kudhibiti usafirishwaji wa fedha za kigeni zinazopatikana hapa nchini, ili kulinda nguvu ya shilingi yetu, hivyo kuimarisha uchumi ambao utatuhakikishia maisha bora kwa kila Mtanzania.
Inawezekana.
Monday, November 06, 2006
Imetokea majuzi kwa mkuu wa mkoa wa tabora, mtoto wa mjini Dito amemuua kwa kumpiga risasi dereva wa daladala kwa kuwa tu jamaa aligonga gari la mhe. huyu lililokuwa likiendeshwa upande wa watembea kwa miguu. Hii ya kutembea kwenye service road si ishu yangu bali ninauliza hivi kweli kuna uhalali wa kiongozi wa serikali kama Dito kutumia bastola yake kumtaka dereva ashuke garini! na polisi wanatuambia eti ililipuka kwa bahati mbaya!
Naogopa sheria isije ikafumba macho. Tusubiri
Monday, October 30, 2006
Kwa muda mrefu sasa wanachuo wa MNMA wamekuwa wakikosa ni wapi wanaweza kusemea na maoni yao kueleka kwa wengine.
MASO serikali ya wanafunzi imeanza kazi ya kuwaunganisha wanafunzi waliosoma katika chuo hiki na wale wanaosoma sasa kwa e mail ifuatayo;
masomnma@yahoo.com
Ukiwa kama mdau wa serikali ya wanafunzi hapa MNMA unaombwa kuchangia kwa kushiriki kuandika mambo mbalimbali kwa kutumia anuani hiyo. Kumbuka uwanja mpana unakuja hivi karibuni
Sunday, October 29, 2006
Msomaji wa machweo, usitishike kusoma kchwa hapo juu kwani nahisi ni kigeni sana kwako.
MASO-MNMA ni kifupi cha jina la serikali ya wanafunzi wa chuo cha kumbukumbu ya mwl. Nyerere.
Kwa mwaka huu wa masomo2006/07 maso iko chini ya rais Hasaan Masudi, na moja ya malengo makubwa ya serikali hii ni kuwaunganisha wanafunzi wote si wa memorial tu bali wa dunia nzima kwa kuingia katika dunia ya blog.
Kwa sasa tegemea makubwa toka katika blog hii itakayokupa mengi toka kwa wanzuoni wa MNMA. Blog hii itakuwa chini ya wizara ya habari inayoongozwa na Obe Mashauri
Hivi karibuni waziri Mramba aliutangazia umma wa watanzania kuhusu madiliko katika kiwanja cha kimataifa cha dar es salaam. mabadiliko hayo ni katika sehemu moja muhimu sana nayo ni ya utambulisho wa mgeni kujua hapa ni wapi na mwenyeji kujivuna kwa kuwa na utambulisho huo.
Mramba na timu yake wanasema kwamba kutokana na sababu za taratibu za kimawasiliano, kiwanja cha ndege cha dar maarufu kama Mwalimu Nyerere international airport sasa kitakuwa kinaitwa Nyerere IA.
mmmh! hii kweli ndo kasi mpya inayohubri mabadiliko makubwa kwa watanzania na mabadiliko haya ndiyo tunayoyaona sasa, yaani watu kwa utashi wao tu wanaamua kubadili jina la kiwanja hiki kwa kuwa tu wazungu hawawezi kutamka jina mwalimu!
Huu ni ulimbukeni na kama anavyosema msanii wa parapanda Mputo katika ghani zake 'salamu zangu' kuwa msikihubiri kiswahili kwa kukitukuza kingereza, kwani kwa miaka yote jina la nyerere shurti lianze na mwalimu na hapo kila mtu duniani hatohoji kwamba huyu mwalimu ni nani. Alijulikana dunia nzima na harakati zake zinazofundishwa kila kona ya dunia hii.
Kuondoa jina mwalimu kisa tu kuna wachache wanapata shida kutamka ni sawa na kusema JFK IA libadilishwe na kuwa unavyotaka wewe. Mbona kuna majina ya viwanja vya ndege si Africa tu bali na sehemu mbalimbali duniani ni magumu si kutamka tu bali hata kuandikwa lakini ndiyo yanayobeba viwanja hivyo.
wanamachweo wanategemea waziri na wizara yake itafanya kama watanzania wanavyohitaji bila kuhoji kwa nini!
na kwa kumalizia kwa watu wenye mawazo kama ya Mramba ni kwamba huwezi kusema nyerere ukimaanisha mwl Nyerere tunayemfahamu sisi watanzania na watu wote duniani, labda kama mnataka kutueleza kuwa jina hilo halina maana sasa.
Monday, October 09, 2006
Ni asubuhi ya tarehe 09/10/2006 kilamwanachuoamekwisha jiandaa tayari kwakwenda darasani,mara rais wa serikali ya wanafunzi wa chuocha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ndugu Hassan J. Masoud anaitisha kikao na wanafunzi wote katika ukumbi wa mikutano.
Hili si jambo la kawaida kwani inaashiria kuna kitu kikubwa wanachuo wanapaswa wahabarishwe, naam, maskio ya kila mmoja yanasubiri nini kitasemwa pale ukumbini na kila mtu yupo kimya. Rais anaanza kuongea ni tangazo la msiba, Msiba mzito wa kaimu naibu mkuu wa chuo ndugu O. K. Temwende
Ni majonzi chuoni na kila mtu haamini kwamba mtu waliyekuwa naye siku moja kabla ametutoka. Kila mmoja anasema analojua na aliloona, wengi tuliongea naye siku ya ijumaa kuhusu tatizo la ada, wengine wakawa naye katika bar ya chuo.
Najua wapo wengi wanaoweza kusema mengi juu ya mwanataaluma huyu, nami pia kwa muda wa kama mwaka mzima tangu nijuane naye chuoni nina mengi yakukumbuka na kujiuliza na kama si kukilaum kifo kwa ukatili uliofanya juu ya mwanazuoni huyu na kada mwaminifu wa chama cha mapinduzi.
Temwende alisoma shule ya Ndanda sekondari zamani sana ikiwa chini ya wabenediktini wa Ndanda shule ambayo miaka ya 90 ilichukuliwa na serikali ambapo nami nilipata elimu ya juu ya sekondari miaka ya 2000. Alipata elimu ya juu katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi na ninachoweza kukumbuka ni pale alipokwendakuchukua masomo ya juu katika moja ya nchi zakisosharist akiwa na A. Mrema kada mwingine wa CCM enzi hizo ambaye sasa ni Rais wa TLP
Darasani marehemu Temwende atakumbukwa kwa kuwa muwazi na siku zote alisistiza umakini na kushirikiana katika shughuli za kimasomo, alisikiliza tatizo la kila mmoja na hakusita kutoa ushauri kwa yeyote aliyeuhitaji.
Marehemu Temwende aliyezaliwa mkoa wa Mttwara alikuwa ni mwandishi mzuri wa makala na kwa wasomaji wa magazeti na hususani wasomaji wa magazeti ya propaganda ya CCM watakumbuka makala zake nzito zilizokuwa zikitolewa wakati Tanzania ilikuwa katika kipindi cha kusaka maoni uwepo wa vyama vingi katika nchi hii.
Temwende alikuwa na dhamana kubwa hapa chuoni na jinalake litabaki katika kumbukumbu za chuo kwani ni yeye aliyeongoza jopo la wahadhiri wa MNMA katika mchakato wa kukifanya chuo kuwa chuo kikuu na hivyo kutoa shahada. Alifanikiwa na matunda yake hakuna anayeyatilia shaka kwani yanaonekana. Alikuwa ni mtu wa vitendo kuliko porojo na propaganda zisizozalisha.
Kuna mengi ya kuandika juu ya marehemu Temwende aliyefariki wakati akiwa njiani kupelekwa hospitali baada ya kuugua ghafla na kukosa pumzi akiwa nyumbani kwake maeneo ya kigamboni jirani tu na ofisi zake za kazi.
Imetangazwa tuna mapumziko ya msiba lakini mambo aliyoyanya marehemu juu ya chuo na kwa kila mmoja aliyemzunguka hayatafutika na hata wengine kujilamu kwamba kwanini amekubali kufa kama padri Karugendo alivyomlaum profesa S. Chachage kwa kufa ilhali kazi waliyokuwa wameipanga kuifanya haijakamilika na kwa kuwa maisha yanaendelea, kila mtu baadaye atakuwa na furaha na pale Temwende alipokomea basi ndipo tutakapoanzia.
Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa
Pumzika kwa Amani mpendwa wetu Omar K. Temwende
Saturday, September 30, 2006
Baada ya Sauper kutuonyesha jinsi tunavyokula samaki mabaki, rais alipiga sana kelele na kuungwa mkono na kila mtu ambaye kwake Darwin9tmare ilikuwa ni uongo kwa kuwa tu kasema raia namba moja.
Sasa kuna hii filam ya IRIN inayoitwa GEM SLAVES Tanzania's Child Labour yaani kwa kiswahili rahisi "utumikishwaji wa watoto katika migodi" filam hii imechukuliwa huko Mirerani wakionyeshwa wanaapollo na 'nyoka' wakifanya kazi ngumu za kutafuta tanzanite wasiyofaidika nayo.
Tumezoea kuandamana na sasa tuusubiri wakazi wa A-town waende barabarani kuilaani filam hii. na cha mno tusubiri rais atakapoenda kuongea na wazee wa arusha atasema nini, kwa kuwa atakachosema kitakuwa ni sahihi kwa watu wanaofikiri kwamba atakalosema ndilo sahii basi tujiandae kuunga mkono hata kama hatujaiona filam yenyewe kama ilivyokuwa kwa wale 'wazalendo' wa mwanza walioandamana kumpinga Sauper bila kuiona hata 'mapanki' yenyewe
Nadhani ni kipindi kimepita tangu niweke kitu kipya gazetini. Wengi pia mmekuwa mkiniuliza kwa sms tatizo nini mbona sionekani tena gazetini au ndo kuchoka kwa kazi ngumu ya kuandika. NO. Niko likizo na maeneo niliyopo mtandao ni tatizo na hata ukipata nafasi katika intanet gharama wanazotoza ni kubwa ukizingatia mtoa huduma yupo peke yake 'monopoly'. kwa sasa nimepata nafasi hii kwani niko jijini kwa shughuli maalum.
Wasomaji wangu kaeni mkitambua kuwa nipo na blog hii haiwezi kuwaacha peke yenu
Monday, August 07, 2006
Watu wanayala sana na hao sato anaowasema wanaliwa na watu wenye uwezo kama wale waliompotosha kwa kusema kuwa wakazi wa mwanza hawali mapanki, wasaidizi wake wamemwingiza mkenge kwa nia tu ya kulinda vibarua vyao.
Mapanki ndo kitoweo cha wengi hasa waliovijijini.
Hii ndo hulka ya viongozi wengi, wanafikiri wao wanapokula vizuri na kusaza nasi twala na kutabasamu.
Sauper hajakosea hata kidogo kila alichokionyesha ni sahihi kwa sisi tunaoijua mwanza na vijiji vyake
Saturday, August 05, 2006
Swali hili linatokana na hatua aliyoichukua mkuu mpya wa mkoa wa Dar es salaam bwana Kandoro.
Mkuu huyu baada ya kupewa rungu la ukuu wa mkoa muhimu wa kibiashara nchini tanzania alikimbilia maeneo ya manzese uwanja wa fisi na kuwatimua mabinti wadogo wanaofanya biashara ya kuuza miili (yeye anaiita ukahaba).
Siungani na watu wanaoshabikia kuwepo kwa mabinti hawa maeneo haya kwani licha ya kuwa umalaya/ukahaba si kitu kizuri kwa dunia ya sasa yenye gonjwa la ukimwi lakini wengi wa mabinti hawa ni wasichana wadogo kiumri(wengi wako chini ya miaka 18 miaka ambayo ni ya mtoto kuwa shule akitafuta elimu).
Sasa wamefukuzwa maeneo haya na wengine wamefikishwa mahakamani ambako mahakama imewaachia kwa kuwaona kuwa hawana hatia (ushahidi ni mgumu zaidi ya kumfungulia mtu mashtaka ya uzururaji). Kwa maana hiyo mabinti hawa wamefukuzwa toka maeneo yao na kutakiwa waondoke kwenda haieleweki wapi na wakafanye nini kwani sasa hawatakiwikujihusisha na umalaya/ukahaba tena.
Sielewi kama mkuu wa mkoa alikuwa anatafuta jina katika kurasa za mbele za magazeti yetu ama ni kasi mpya na nguvu mpya!
Unaweza kujadili suala hili, je kuwafukuza hapo ndilo suruhisha au suluhisho ni kuwaandalia mbiu nyingine za maisha kama KIWOHEDE wanavyofanya pale Buguruni. Pia ni lazima jamii ijue kuwa si Uwanja wa Fisi tu kunakofanyika uchafu huu, ni sehemu nyingi sana hapa dar na katikamiji mikubwa mingine kama Mwanza, Mbeya na Arusha
Wakati akiwaapisha wakuu wapya wa wilaya za jiji la dar aliwataka kuhakikisha kuwa wanafanya kazi zao na kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa katiba. Huu kila mmoja anauelewa ili alinde kitumbua chake
Lakini amewakasirisha wakazi wa mabondeni ambao wamekuwa ni sugu na mara zote wameishinda serikali mahakamani kuhusu suala la kutoka katika maeneo haya hatari hususani maeneo ya jangwani.
Kilichonifanya niandike jambo hili ni ile kauli ya wakazi wa jangwani kwanza kumhusu Kandoro kama yeye na yeye kama mkuu wa mkoa, jiji la dar
Wengi walimweleza kama mgeni ambaye hata mjini hajakaa halafu anaanza kuwaletea longolongo wakati wao wamekuwa pale kwa miongo na watoto wao wanasoma muhimbili primary huku wakipata huduma ya uhakika ya matibabu toka hospitali ya taifa Muhimbili halafu leo Kandoro apange kuwaondoa!
Mgosi (Makamba) kashindwa atakuja yeye! tusubiri tuone kwani kasi aliyokuja nayo ya kuwatimua mabinti pale uwanja wa fisi inaweza kuwa juu ya wakazi wa mabondeni
Tuesday, July 25, 2006
Hata wewe ni mpigadebe
Haya kaandika mwandishi makini wa makala katika gazeti la kila wiki RAI, huyu ni faza Priva Karugendo, nisipoteze kusema alichosema hebu soma mwenyewe na uone alivyoandika na kwa kauli yake hatakomea hapokwani ataandika mengi kuhusu hili(wakati anaandika alikuwa anawahi ndege toka mwanza kuja dar, huyu ni mwanaharakati wa mambo ya kijamii, na mwanafalsafa wa kileo,ukisoma makala yake anayomlaumu Chachage kwa kufa utaelewa ninachokisema) na hivyo usiache kusoma suala hili katika blog hii
Ndugu yangu, Asante sana kuandika. Leo hii nitakuwa Dar. NitaondokaMwanza, na ndege ya saa mbili usiku.Ukipata nafasi uniite kwenye simu. Lakini Juma lote nitakuwa ninakimbia huku na kule. Unajua, Watanzania wote ni wapigadebe! Maana yake ni kwamba: Hatufanyi uzalishaji. Mtu ananunua shati Kampala, analileta Magu, Mwingine ananunua shati lilele na kulipeleka Mwanza, wa Mwanza, analipeleka Moshi, Arusha hadi Dar. Yote hayo ni sawa na kupiga Debe. Mpigadebe, anapata pesa kwa kumleta mtu kwenye gari, ambalo hata kipofu anaweza kujua kwamba linaelekea Mwanza! Anapata pesa bila kuzalisha chochote. Mwisho wa mwezi anakuwa na pesa kuwazidi watu walioajiriwa ofisini!
Umeyaona haya, mengi yaja
Nimeamua nichokoze mawazo yako wewe mwananchi kuhusu suala la wapigadebe katika vituo vya mabasi ya ndani ya miji (daladala kwa dar na express kwa mwanza)na nje ya miji (yale yaendayo mikoani)
Hawa ni vijana wenye umri wa kati kuanzia miaka 15 hadi45 yaani ni kama marehemu profesa Chachage alivyopenda kuwaita vijana wa kizazi cha dot.com. Aliwaita hivi kwa sababu moja kubwa bayo ni kwamba wengi wa vijana wamezaliwa baada ya tz kupata uhuru yaani baada ya 1961 na wamekulia katika kipindi ambacho nchi imeshuhudia mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni,
Tukirudi kwenye mjadala kuhusu kundi hili ambalo sasa linakua kwa kasi mpya na nguvu ya jumbo, hivi ni sababu zipi zinasababisha hali hii itokee
Je jamii inahusika na jamii ni nani kama ni hivyo! serikali na taasisi zake ina mkono katika hili!
karibu utoe maoni yako!
Saturday, July 22, 2006
Nimeupata toka kwa rafiki yangu anayeblog pia
Utenzi wa Prof Issa Shivji aliouandika juu ya kifo cha ghafla cha guru la sayansi ya jamii prof Seithy Chachage
.Ndugu yangu
Rafiki yangu
Kamaradi Chachage:
Nani kasema umetuacha?
Eti umefariki!
Kwani mwili ndiyo maisha?
Maisha ni fikra. Maisha ni vitendo.
Maisha ni ubinadamu.
Fikra zako,
vitendo vyako,
ubinadamu wako,
utadumu.
leo, kesho, keshokutwa na milele.
Vitendo vyako tutavienzi,
ubinadamu wako tutauiga,
fikra zako tutazieneza.
Msomi wa Afrika,
mteTEzi wa wanyonge,
mshabiki wa fikra za kitabaka,
tabaka la wavujajasho.
nimetumwa.
Nimetumwa na Wasomi wenzako wa Afrika kupitia CODESRIA nikuletee Salaamu zao.
Wameniambia, nikuage.
Nimekataa.
Sikuagi.
Nitakusindikiza tu.
uwaone Wazee Wako,
majirani zako,
watu wema wa Njombe.
Uchanganyike na viumbe wa ardhi na bahari,
viumbe visivyo na ubaguzi,
mipaka,
unyonyaji,
ukandamizaji.
Uwashawishi,
wafundishe wanadamu maana ya ukombozi.
Kama ulivyokuwa unatufundisha sisi daima.
‘Ewe Issa,
kwani,
Shivji siyo mwana wa adamu?’,
Ukanitania,
Ukichota kutoka hazina ya ucheshi wakO bila uchoyo.
"Umejipachikia majina haya yote ya Miungu! MLIMBIKAZI, WE ISSA!’
"Mungu wa Waislamu na Mungu wa Wakristo,
Mungu wa Wahindu na Mungu wa Wasambaa.
unataka wapigane?
wachinjane.
Eti moja ni –a, mwingine ni –ji!’
"Futilieni mbali ushenzi wenu wa kubaguabagua!’,
ukakasirika.
"Unganeni kujikomboa",
umetusihi, "kutoka kwa makucha ya ubeberu na ubepari,
unyonge na udhalilishaji.’
Buriani ndugu yangu,
Buriani rafiki yangu,
Buriani Kamaradi Chachage.
Ufikesalama.
Upumzike na Viumbe visivyonyumbishwa na vituko vya Wanaadamu.
Nakuahidi.
Nitaufikisha ujumbe wa maisha yako.
Kwa WanaUdasa,
Kwa WanaCodersia.
Kwa Wana wa Tanzania,
Kwa Wana wa Afrika………………….Buriani………..
Wednesday, July 12, 2006
Hakika nakosa maneno ya kuandika kuhusu kifo cha ghafla cha guru la midahalo ya kisomi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
Inahitaji kuwa na nafasi kubwa kuweza kuandika kile ninachofahamu kuhusu mtaalam huyu wa sayansi ya jamii na mwandishi wa vitabu.
Nakikumbuka kitabu chake ambacho kinapingana na utandawazi usio haki unaopigiwa chapuo na viongozi ambao nia yao si ya jamii nzima bali ni kujitajirisha peke yao na watoto wao, kitabu hicho kinaitwa Makuwadi wa Soko Huria
Si kwamba watanzania tumepoteza lulu bali afrika nzima na wote wanotaka usawa duniani wamepoteza hazina kubwa lakini kupitia maandiko na machapisho yake hakika watazaliwa kina chachage elfu
Nakumbuka msemo wako wakati ukihojiwa na mtayarishaji wa kipindi cha luninga Sema Usikike ulisema neno ambalo sitokaa nilisahau " hakika kuhusu ujambazi kuna sehemu imeoza na wala si sahihi kusema kwamba umaskini ndo chanzo cha ujambazi, jamii na viongozi wa serikali wajiangalie wapi kuna mgogoro unaozalisha wimbi la majambazi na wapiga debe"
Buriani Pro. Seithy Chachage
Thursday, July 06, 2006
Linaweza kuwa kama swali la mtu aliyechoka kufikiri. Nimewahi kukuandikia kuhusu kupanda kwa ada hapa chuoni kulikotangazwa na kaimu mkuu wa chuo kama ilivyoamliwa na kikao cha bodi ya chuo hiki chenye jina la muasisi wa taifa hili na aliyekuwa anataka kila mwanachi asome maana yake ni kuwa ada ya masomo iendane na uwezo halisi wa mtanzania wa kawaida.
Sio vibaya kujifikiria kitu ambacho wenzako wanaweza kukufikiria vinginevyo lakini kwa suala la ada kupanda hapa chuoni linamgusa kila mtu anayetoa pesa ili kupata elimu. Inawezekana kabisa waliopandisha ada (bodi) walikuwa na sababu kubwa na za msingi huku wakisaidiwa na utafiti walioufanya kana kwamba kutoza ada kubwa ndo kuonekana chuo bora
Lakini inawezekana kuwa wao kama wao na mishahara yao hawaoni tatizo na ada hii mpya kwani kama watu wanakaa kikao kwa siku na kulipana posho sawa na mshahara na marupurupu ya mwezi ya askari ada hii kwao ni ndogo na ni aibu kuilipa kana kwamba mwalimu alikuwa anafanya biashara ya elimu.
Pia labda bodi ilijua kwamba rais ataongeza mishahara na ndiyo maana ikaamua kuongeza ada ili kutorahisisha maisha kwa namna yoyote na hasa ukizingatia kuwa chuo hiki kipo katika ilani ya ccm katika mkakati wake kukiwezesha na kukikarabati!
Nakaribisha maoni kuhusu suala la kupanda kwa ada. Nenda sehemu iliyoandikwa comment bonyza na andika maoni yako na uyatume. Karibu
Ijumaa iliyopita ilikuwa ni siku muhimu sana kwa wote wanachuo kwani ukiacha wengine waliokuwa wanamaliza mwaka wao wa kwanza wa masomo wengine walikuwa wakimaliza kozi zao za stashahada na cheti.
Ilikuwa ni siku ya maagano huku kila mmoja akiwa na huzuni ya kuachana na rafiki yake na furaha ya kupokea cheti na kuanza mwaka mpya wa masomo bila kusahau ada iliyopanda
Blogu hii inawatakia mapumziko mema wanachuo wa vyuo vyote na ni wajibu wetu kutunza afya
Friday, June 23, 2006
Wakati mwanablogu mkongwe Ndesanjo Macha wa jikomboe.com analalamika kuwa afika si kitu yaani ni sifuri kwa kila kitu anachokitazama yeye na hasa akatilia maanani eti aibu inayozikuta timu zetu ambazo baadhi zimetolewa katika raundi za makundi
Jana Ghana wamemdhihirishia kuwa afica ndiko mpira unachezwa kwani black star waliwachabanga vijana wa Joji Kichaka kwa mabao mawili kwa moja huku ushujaa ukionekana karibu katika kila sekta ya timu ya Ghana hongera kwa wote na hasa kwa mashabiki tuliojitokeza kwa wingi kuwapa shavu vijana wa Africa.
Tunakutana na Brazil! Tutawashinda na ni bora nikasema kama kiungo mahiri wa Ghana Michel Essien alivyosema "tumecheza nao katika under 17 na 21, tunawajua kwani tuliwafunga bila kusubiri uda wa nyongeza" hakika brazil atapigwa bao 3-1 huku Appiah, na Essien wakifunga na Gyan bao kali la kichwa
SHANGILIA GHANA MABINGWA WAPYA WA KLD
Kwa ushindi huu Afrika imepata nafasi moja ya kuwa na timu ya 6 hapo 2010
Ukisoma bila kufanya mitihani sidhani kama unastahili kuitwa msomi japo hili linaweza kuwa na maana nyingine ila kwa mtazamo wa machweo mithihani ndicho kipimo sahihi kabisa cha kumtambulisha mwanafunzi na mtu mwingine
Mitihani inaanza j3 hapa MNMA kwa niaba ya wachangiaji na wasomaji wa mada mbalimbali katika machweo ninawatakia mitihani salama wale wote tutakaokaa na kufanya mitihani hii.
Vilevile ni kipindi hiki ndipo tunaagana na wenzetu wanaomaliza mafunzo yao ya diploma na hivyo tunawatakia mafanikio mema huko waendako kutafuta ajira katika dunia hii ya utandawazi
Thursday, June 15, 2006
Hassan Jani ndiye Rais mpya aliyechaguliwa kuiongoza serikali ya MASO-MNMA baada ya kuwashinda wapinzani wake wawili Rama Warioba na Rehema H, katibu wake bado hajapatikana kwani Emmanuel Ndunguru na Janeth Soka walilingana kura na hivyo bado tunasubiri utaratibu mpya wa kumpata katibu mkuu, Viongozi waliochaguliwa ni hawa hapa chini na wanasubiri muda tu waweze kuapishwa ili kuingia kazini na kufanya kazi
Rais;- Hassan Masoud Jani SSI
M/Rais:- Bado
Waziri wa Fedha: Edward Biashara Baridi EDI
Waziri wa Afya: F Katanzi GI I
Waziri wa Ulinzi na Makazi: Adam R. Kikono SSI
Waziri wa Michezo na Mahusiano ya Nje: Samwel Mhinga SSI
Waziri wa Habari: Obeid M. Mashauri SSI
Kama ilivyo ada kwa watanzania kazi yetu sisi ni kushabikia tu timu za wenzetu. Najua sasa wengi wetu tunajiita Waghana, Angola na wengine tunajiona tuna ukoo na kina kafu! Ronaldo. Hizi tabia ndo zetu na wala hatuna haja ya kujiuliza ni kwanini hatuioni timu yetu ikishiriki katika kombe kubwa kama hili japo mara moja.
Tushiriki ya nini bwana kama watu kombe lilishaletwa tena lile orijinali na tukapiga nalo picha na kisha rais akalibeba kuonesha kwamba sisi si wageni katika suala zima la kabumbu.
najua tumejigawa lakini swali tunalopaswa kujiuliza ni nini tunajifunza kwa kombe hili ukizingatia timu kama Angola inashiriki na kuvitoa jasho vigogo! Tanzania ni nchi ya amani lakini haipendeza kuona ndani ya amani hakuna nafasi ya kujitangaza na sasa soka licha ya kutoa ajira ila ni utalii tosha na nchi kupata wawekezaji katika sekta mbalimbali
Nilitaka kusahau mimi ninashabikia timu hya Ghana na nikiwa kama mchezaji wa soka nafasi ya kiungo mzuiaji na mara mojamoja kufunga ninapendezwa na uchezaji wa Essien, wewe unashabikia timu gani ukiacha Brazil ambayo ni timu ya wote
Furahia michuano mikubwa hii ukijiuliza utafanya nini Tanzania nasi tuweze kushiriki japo raundi ya kwanza
Sunday, June 11, 2006
Mpenzi msomaji wa gazeti hili, juma lililokwisha nilikueleza kuhusu mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu Nyerere, uchaguzi ulifanyika siku ya ijumaa kuanzia saa kumi jioni na mpaka kufikia saa 12 jioni kazi ya kupiga kura ikawa imemalizika wakasubiriwa mawakala waanze kuhesabu kura 'kula'
nafikiri unajua kuwa nilikuwa ni mmoja wa wagombea nikigombea nafasi ya uwaziri wa habari (usishangae hapa MASO uwaziri unagombea, hawateuliwi yaani wote ni kama maraisi) na nilikuwa na nashindania nafasi hii na mtangazaji wa television Zanzibar.
katika uchaguzi huu nafasi zilizokuwa na ushindani mkali ni nafasi ya urais ambayo ilikuwa na wagombea watatu akiwamo mwanamke mmoja pekee aliyejitokeza ( Anna Senkoro!!!) na vivyo hivyo kwa nafasi ya ukatibu mkuu na makamu wa rais (mtu mmoja anakuwa na cheo chenye nyadhifa mbili).
Upande wa nafasi za mawaziri wizara zilizoshuhudia upinzani mkali ni wizara ya michezo na mahusiano ya nje pamoja na wizara ya afya na kafteria.
Najua unadhani nilishindwa na ndio maaana nazunguka tu bila kukupa matokeo hususani ya wizara niliyogombea.
hakuna kitu kizuri kama kusoma ishara za nyakati na kuzifuata, usipozitii basi yatakayokukuta unaweza ukatafuta wachawi na sababu chekwa huku wapiga kura wakiwa pembeni na tabasamu zito wakikuangalia jinsi unavyohangaika kutafuta chanzo cha wewe kushindwa.
Mpinzani wangu, dada mrembo anayepaka rangi ya shaba nywele zake huku tabasamu tamu likiwa usoni kwake kwa wale anaowafahamu alisoma alama za nyakati na akaona hakika hata angeingia katika mbio hizo basi ingekuwa mashindano ya chui na kobe ambapo mshindi anajulikana.
Siku ya mwisho kabisa alijitoa na nikawa mgombea pekee na ushindi nilioupata siwezi kuuita wa tsunami kwani janga hili linaendana na maafa ila tambua kwamba nilipata ushindi mtamu na ni kura 11tu zilimchagua'mwenzangu' na hizi ni kura mhuhimu kwani zinanifanya nijitambue mimi ni nani na ninapaswa kufanya nini si kwa wale walionichagua tu bali kwa wale muhimu wachache walioamua kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa mpinzani (niruhusu nmwite kivuli)
Bado tunasubiri nafasi moja kwani wagombea katika nafasi katibu mkuu na makamu wa rais hawakufikisha nusu ya kura ili mshindi aamuliwe na hivyo uchaguzi wao jumanne jioni
Tegemea mazuri katika mchakato huu mapema kwani nitakuletea orodha ya wagombea na kura zao.
tafadhari kumbuka gazeti hili sasa liko chini ya wazir wa Habari-MASO
Saturday, June 03, 2006
Nilikuandikia wiki jana na kukutaarifu juu ya kupaa kwa ada kwa wanachuo wa MNMA.
Jana Ijumaa kaimu wa mkuu wa chuo akaitisha kikao cha wanafunzi na ajenda kubwa ilikuwa ni kututangazia ada mpya ambayo ni tshs 820,000/= toka laki sita, yaani ongezeko la tshs220,000/=
Shabaaaash!!!!!!
Ongezeko hili ni kutokana na kikao cha bodi kilichoketi na kufanya utafiti wa ada katika vyuo vingine! Vyuo vingine vinavyosemwa kuwa ni adfa kubwa ni vile ambavyo havina mkono wa serikali kwa asilimia mia kama kilivyo vhuo hiki.
Kuna maoni mbalimbali kuhusu ongezeko la ada hii,
Nitakuandikia
Wednesday, May 24, 2006
Huu sio kama ni uzushi bali ni utabiri halisi.
Chuo kimeamua kuongeza ada kwa wanafunzi wa diploma kisa eti wanatoa mafunzo ya komputa.
kweli jina la Nyerere sasa linatumiwa kibiashara
Nitakuandikia tena kwani kama watu tshs 600,000/= nanga inapaa itakuwa hii 800,000/= wanayopanga au ni kwa ajili ya masirahi binafsi ya kujilimbikizia pesa kwa mgongo wa wavuja jasho!!
tangazo hili likitolewa hakika mwalimu atajigeuza alipopumzika
More 2 come
Nauliza hivi kwa kuwa kila ifikapo tarehe kama ya leo kila mwaka, ofisi huwa zinahaha kutangaza wafanyakazi bora. Sijui wanatumia vigezo vipi.
Muda wote wachapakazi ndo wanakosa nafasi hizo na wanaopata ni wale wanaopendwa na wanaowateua; iwe manajimenti, ofisa mtendaji mkuu na wote wanaofanana na hao.
Sasa mimi nasema hakuna cha mfanyakazi bora wala nini. Wote n i watumishi tu na mtindo huo wa kuwepo wafanyakazi bora unadumaza utendaji wa kazi wa watu wengine na ndiyo maana nchi zetu haziendelei.
Nimemaliza
Tuesday, May 23, 2006
Usije ukafikiri ninachokuandikia hapa ni utani. 'Kaimu' rais wa MASO ametoa tangazo la kuwataka wale wote wanaotaka kuingia katika mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi hapa chuoni basi wachukue fomu katika ofisi za MASO!
Kila mmoja maeliona tangazo hilo lenye sahihi tu ya rais bila muhuri wa MASO yaani kwa ufupi kama usipokuwa makini tangazo limekaa kama barua tu unayoweza kumwandikia shangazi yako. Kila mtu anajiuliza hivi kweli uongozi hauna muhuri na kama hauna muhuri na kama hauna basi huu ni uhuni na haupaswi kuwepo.
Juzi nilikuandikia kuhusu suala la wanachuo wachache waliokuwa wamechelewa na chuo kupitia kwa dean! wakaamriwa wafukuzwe na kama watapenda basi warudia mwaka wa masomo.
Wengi wa hawa waliochelewa ni wanafunzi wa mwaka wa pili ambao ni kama wamebakiza siku 26 wamaliza kozi na kutunukiwa diploma yao kama watakuwa wamefaulu.
Mapema leo asubuhi wamepewa barua za kuondoshwa chuoni zikiwa zimesainiwa na kaimu wa naibu wa mkuu wa chuo.Barua hizo hazina rejea hata moja na kuonyesha kosa la mhusika, zimemshangaza kila mmoja hata yule asiyekuwa na elimu ya sheria kifupi ni kwamba zinakanganya sana.
mkanyiko huu hauishii kwenye barua tu kwani wakati wa kipindi cha tatu leo mchana Naibu wa mkuu wa chuo hiki cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, aliwaita wahanga wa msala huu na kuwasamehe, tena kwa msamaa usio na barua.
Inachanganya kuona kwamba mtu umemfukuza kwa barua na unamrudisha kwa kutompa barua, hii haina matatizo ya kisheriakweli au ndo mtindo wa mazoea kwamba mimi ndo kila kitu na ninachosema ndicho kifanywe hata kama kuna bodi yenye dhamana ya chuo hiki
Sunday, May 14, 2006
Inashangaza sana kama unahubiri kitu bila kuwashirikisha unaowahubiria.
Hivi nikitoka likizo ninaripoti kwa nani au ni kutafuta visa tu. Nitaandika tena kuhusiana na hili kwani kuna mwanafunzi amerudishwa nyumbani kisa amechelewa kuripoti na mbaya zaidi huu ni mwaka wake wa mwisho. Tuelezwe tulipoti kwa nani au kuna kingine nyuma ya pazia
Saturday, May 06, 2006
Imetoka katika gazeti la Mtanzania April1 eti kuwa kaimu msajili wa chuo cha MNMA amemkaba na kumpora mwanachuo. Hii si habari njem a kwa chuo chenye jina la muasisi wa Tanzania na kama haina ukweli basi ni vizuri tukapewa ukweli halisi ili kuondoa mawazo na maneno yanayoibuka bila mpango. UPOOOOOOO!
Imetoka katika gazeti la Mtanzania April1 eti kuwa kaimu msajili wa chuo cha MNMA amemkaba na kumpora mwanachuo. Hii si habari njem a kwa chuo chenye jina la muasisi wa Tanzania na kama haina ukweli basi ni vizuri tukapewa ukweli halisi ili kuondoa mawazo na maneno yanayoibuka bila mpango. UPOOOOOOO!
Ndugu msomaji nimeamua kuipandisha kurasa hii ambayo niliiandika mwaka jana wakati chuo hiki kikiwa hakina huduma acha ya kompyuta kwa wanafunzi bali hata mtandao kwa ajili ya kuwasaidia katika kutafuta 'material' kulingana na kozi wanazosoma.
Hali sasa ni tofauti kwani milango ya chuma sasa imefunguliwa na kompyuta zipo huku wasimamizi wa maktaba wakiwepo kusaidia wale wote wanaotatizwa na teknolojia hii. Haya ni mabadiliko na tunajua kuna mengi yanakuja. hebu soma nilichoandika kipindi hicho ambacho leo ni historia
Ukifika na kuuliza ni hakika utaambiwa wanachuo wanasoma kompyuta kwani ni kweli kabisa kuna madarasa mawili yaliyojaa kompyuta na bahati nzuri nyingine zimeunganishwa katika intanet. Majibu utakayopewa ukaridhika na upande mmoja basi ukweli halisi huwezi kuupata na utaondoka ukiwa na furaha ya kwamba kweli chuo kimebeba jina linalostahili hivyo nacho kinastahili.
Labda nikuonyeshe upande wa pili wa majibu uatakayoyapata kutoka kwa walengwa wenyewe, wanachuo. Hakuna mafunzo ya komyuta na hakuna mwanachuo anayeruhusiwa wacha kuzigusa kompyuta zenyewe bali hata kusogelea karibu a milango miwili ni shida, milango yote inalindwa na mageti ya chuma na kufuli maalum yaani kama za benki.
Inashangaza sana kwa chuo kama hiki kutowaruhusu wanafunzi kutumia vifaa hivi kwa ajili yua kujisomea na kufanya kazi nyingine za kitaaluma kwani hakuna ubishi kwamba intaneti inamwezesha msomaji kusoma vitabu vingi na vya wakati huu.
Juzi nimekutana na rafiki yangu namfahamu tangu tukiwa A-level, yupo hapa chuoni na alikuwa library akitafuta kitabu cha Rural Sociology ambacho hakipo katika 'shefu' za maktaba, alisikitika na nikamwona akimjongea mhusika wa library kujaribu kumwomba agoogle' apate japo nini cha kusoma
Hii haipendezi na hasa kama mtu mzima anapohubiri mabadiliko bila kubadilika akitegemea anaowahubiria wabadilike! Inawezekana tu kama wanaohubiriwa wataamua kumbadilisha yeye kwanza na bila kujali watatumia nini kumbadilisha
Nadhani ujumbe huu ni salamu tosha kabisa kwa MASO kutambua kwamba wapo kama daraja la kutusemea sisis tunataka nini, na si kukaa tu wakilipana posho kwa pesa tunazokatwa kama ada ya chama
Pia uongozi hasa kamati ya taaluma ambayo naamini kabisa inaongozwa na mtu anayependa wanafunzi wajifunze vizuri katika mazingira rafiki uatalifikiria jambo hili
Tuesday, April 18, 2006
Naam, mambo yamekwisha anza na mapema tu kipyenga kikapulizwa 18/04 na kama kawaida malekchara wakaanza kumwaga lekcha! Unashangaa kuna darasa lilikuwa mahudhurio ya wanafunzi 5, hii haijakaa mwake jamani msiuweke kwani imeshatangazwa kwamba siku ya kufungua na masomo kama kawa.
Wahi usiuweke, duh! inaonekana nyasi zilizozunguka mazingira ya chuo zinapenda sana mvua kwani zilivyoota uatashangaa na laiti kama makwanja yangekuwa yanafanya kazi basi zingeweza kufyekwa kwa ustadi ili kuzifanya zivutie zaidi, nadhani kila mtu analiona
Monday, April 17, 2006
Kama kuna mji ambao wanafunzi wanakuwa na wakati mgumu wa kwenda na kutoka shuleni ni Dar. Hii ni kwa sababu namba kubwa ya wanafunzi hawa wanasoma shule za kutwa zilizo mbali hivyo kuwafanya wategemee usafiri wa daladala kwani serikali ya Dar haitoi maelezo ya kutosha kuhusu mradi wa magari ya wanafunzi.
Juzi nimepanda daladala na nikashuhudia sheshe zito kati ya kondakta na 'dent' Hakuna aliyetaka kushindwa kila mmoja alikuwa ni mbabe kwa mwenzake konda anataka nauli ya mtu mzima na denti anatoa 50/=na kitambulisho cha shule anayosoma. Tafrani inaishia kwa abiria kuwa upande wa dent na kila kitu kikawa kama kawaida.
Inanikumbusha wakati ninasoma sekondari na siku moja nikampa konda50/= na kitambulisho cha shule niliyosoma Ndanda (Naleo Pasona en grata, Mwaimu, Limbu, na wengi najua mnaikumbuka shule hii) kumpa kitambulisho akashangaa na kuniuliza kama Ndanda Kosovo ( mwanamuziki wa wajelajela) kama ana shule. Sikutaka kumjibu kwani ni mazoea kwa konda na denti kila mtu kumtegea mwenzake nani aanze kutoa kashfa inayofuatiwa na vita kali ya maneno baini ya wawili.
Bahati nzuri mzee mmoja wa makamo akamshangaa konda kwa kutofahamu hata shule ambayo rais mstaafu Ben Mkapa aka Mr Clean alisoma, konda ulimi ukakatwa nami nikatulia kwa kujiamiani kituo kilichofuata nikashuka.
Nadhani ni wakati muafaka kwa wanadar kujadili ni kwa vipi tatizo la usafiri wa wanafunzi linaweza kutatuliwa pia na mikoa mingine, kila mmoja ashiriki bila kujali ni nani na ana nini!
Jumatatu njema ya pasaka
Saturday, April 15, 2006
Barua ya Kaimu Mkuu wa Chuo cha MNMA ilibandikwa ubaoni ikitoa 'shavu' kwa Mr O. K. Temwende ( Kaimu Naibu wa Mkuu wa MNMA) na kamati yake ya taaluma kwa kufanikisha utaratibu wa chuo kuanza kutoa B.A. Mara zote tunajua wakubwa hupongezana ndani kwa ndani na wakati mwingine mkubwa sana hampongezi mdogo na hatambui mchango wake lakini kwa mara ya kwanza barua ya Dk Magotti inasomwa na kila mtu na wote tunakubali na kuithamini kazi ya Mr Temwende. Bravo Mr Temwende na kamati yako!
Wanachuo wote tunapewa vitambulisho vizuri kabisa ( sina uhakika na ubora wake hususani ile nailoni kuachia na kufanya karatasi kuchanika! nakumbuka jinsi dean of student alivyochachalika kuhakikisha vijana wake tunatembea tukiwa tunatambulika,( unamkumbuka yule jamaa wa SS1 aliyesema kwamba alikamatwa na polisi kitambulisho cha kuazimia vitabu maktaba kikamuokoa! Alikuwa anatoka kuwachangia tbl kuwafanya watoe kodi kubwa kwa serikali na mishahara minono kwa wafanyakazi wakitukutanisha pamoja bushtrekker tehetehete!
Hivi tangazokwamba kuna mafunzo ya kompyuta linatuhusu wote
Saturday, April 08, 2006
Najua kila mtu anajiandaa kwa ajili ya sikukuu mbili kubwa kwa watu wa madhehebu yote makubwa ya dini za kigeni, Waislamu na Wakristo
Najua kabisa kwamba waislamu mtakuwa na maulid ya Mtume na baadaye Wakristo watafungua kwarezima na hivyo kusheherekea Pasaka
Machweo inawatakia sikukuu njema na mkae mkijua kwamba jumatatu chuo kinafunguliwa na usishangae jumanne kukawa na paper si unajua mambo ya kasi mpya na kwa mara ya kwanza
Peace&Love from Geka
Sina hakika na mitihani tuliyofanya kama ilikuwa imeandaliwa kwa umakini wa kina na kwa kuzingatia hali halisi na jina la chuo.
Usishangae kwani kwa sasa kila kiti kiko wazi kwani sheria ya nchi inatamka wazi bila kigugumizi kuwa sasa hakuna chuo kinachoitwa Kivukoni Academy of Social Science (KASS). Cha ajabu kabisa ambacho kwa sababu tu ya mazoea ya watu kushindwa kuhoji ni kwamba mitihani tuliyofanya ratiba ilikuwa inaonyesha kuwa wanaofanya ni wanachuo wa KASS na si wa MNMA.
Ukiachana na ratiba bado karatasi za kujibia zilikuwa na mihuri ya KASS na si MNMA kama inavyotakiwa kuwa kwani shughuli zote za KASS zimerithiwa na MNMA.
Hii inachanganya na wakati mwingine mtu yeyote bila nia ya kutaka kumsema mtu utaona kwamba ni kama uandaaji wa ratiba na upigaji mihuri ulikuwa ni wa kushangaza kwani mitihani imeandikwa MNMA ratiba na karatasi za kufanyia mitihani zinaandikwa KASS, labda inawezekana kabisa kwamba haya matangazo ni danganya toto na MNMA haijarithi chochote toka KASS
Ninakaribisha maoni kama unaweza kuchangia kwa hili bila kumkashifu na kumsingizia mtu.
Najua wengi sasa mtakuwa na hamu ya kujua nini kinaendelea katika chuo hiki kisicho na journal wala gazeti. Tumia blog hii kusema nini unafikiri na toa mawazo yako ya kitaaluma ili kusaidia wanachuo wote kwani chuo ni zaidi ya majengo na wanafunzi
Monday, March 27, 2006
Sunday, March 19, 2006
Nawajua wengi amabo kila wakisikia mitihani baaasi kuumwa si kuumwa na kila kitu kinabadilika yaani wanaweza kusahau hata kuoga.
Ninachukia mitihani lakini si kama ninaiogopa, la , siwezi kuiogopa kwangu mtihani mgumu kabisa ulikuwa ni wa darasa la nne ambapo kila mwanafunzi kipindi kile alikuwa na kitete cha kuingia darasa la tano. Siidharau mitihani hii ila ni kwamba ninataka kuwaencourage watahiniwa wenzangu kwamba kama wao waliomaliza walifaulu kwa nini sisi tushindwe,
Nawatakia mitihani mizuri na mfanye mkiwa na moyo wa kijiamini. Love
Thursday, March 09, 2006
Ni jambo la kushangaza kwamba jumuia ya chuo hiki kilichobeba jina la baba wa taifa la Tanzania Mwl. J. K. Nyerere hakina gazeti la wanachuo. Kila mwenye mawazo yake timamu atajiuliza na kupata jibu lazima awatafute wahusika, nimewatafuta na jibu kutoka kasso halieleweki
Si kwamba hawajui maaana ya gazeti kwa wanachuo la, ni uzembe na mazoea ya labda kwa kuwa library kuna Mtanzania na Rai, Daily Newz na hivi wanachuo wanapaswa wasome na si kuchangia hoja zao katika gazeti lao.
Kwa kuona tatizo hili ninakuomba mwanachuo mwenzangu tumia blogu hii kutoa maoni yako ya aina yoyote ilmradi tu haumtukani yeyote. Tumia lugha yoyote ila ningependa sana kama ukatumia Kiswahili ili na wengine wengi wanaojua maana ya lugha hii katika kuwasiliana wakasoma na kufurahi, kuongeza uelewa na kushiriki katika mijadala mbalimbali ninayoitegemea kutoka kwako.
Nina imani kabisa hata serikali ya wanachuo itakuwa na nafasi ya kuchangia na kueleza yote yanayojitokeza ofisini kwao. Najua matangazo yao mengi wanayatoa kwa kuandikwa kwa mkono lakini kwa kuwa chuo kitaendesha kozi ya kompyuta basi natumaini hali itabadilika na pale ubaoni hatutaona tena tangazo lililoandikwa kwa mkono toka Administration na katika serikali ya wanachuo.
nakukaribisha sana katika blogu hii jisikie huru kutoa mawazo yako yenye kujenga jamii nzima si ya wanachuo tu bali ya wasomaji wote wa ndani na nje ya nchi kwani ni ukweli kwamba blogu haina mipaka na kazi ya kuihariri inahitaji busara ya kutembea na taa mchana
Kwa mara ya kwanza tangu nijisajili kama mwanachuo wa hapa THE MNMA juzi tumekaa kikao cha kwanza huku mkuu wa Principal akiwa mgeni rasmi na katika hali ya kushangaza kabisa Dean of Student akawa ndio kama 'MC'wa kikao hicho.
Nilitegemea lugha itakayotumiwa itakuwa ni ya kistaarabu na kirafiki hasa kwa kikao kama hiki cha watu wenye akili zao wanaohitaji kuelezwa yote yanayoona sawa si sawa kwao.
Nitajitahidi kukuletea yote yaliyojiri katika ukumbi huu wa bush trekker
Muhimu ni kwamba kumbuka kwamba ada inatarajiwa kuongezwa kwa kuwa tu kutakuwa na masomo ya kompyuta