Thursday, April 17, 2008

UNAFIKI WA VIONGOZI WA DINI

Siongelei dhehebu moja ama mawili, naongelea viongozi wa dini zote za kigeni( ambazo hazina asili yake Afrika).

Makanisa yetu na misikiti yetu imekuwa ikipokea misaada mbalimbali toka kwa wafadhili wa ndani na nje. Misaada hii imekuwa ni kwa ajili ya maendeleo ya waumini wote.

Cha ajabu sasa ambacho msomaji unaweza kukubaliana nami ni kuwa, misaada hii imekuwa ikiishia matumboni mwa viongozi hawa ambao unapokutana nao njiani na maneno yao huku wakiosha mikono kila wanapoongea ni tofauti kabisa na matendo yao ya KIFISADI.

Tunapoongelea kuhusu ufisadi kwa viongozi wa serikali basi tusisahau kile kinachofanywa na viongozi wetu wanaovaa majoho na kanzu nzuri
UTAJIRI WA CHENGE

Kama kuna jambo ambalo linaongelewa sana kwa sasa hapa kwetu Tanzania ni suala zima la utajiri wa Chenge ambaye aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali kwa kipindi cha miaka 10 katika zama za Mkapa.

Ni katika kipindi hiki ndipo taifa lilishuhudia uingiwaji mkubwa wa mikataba ambayo leo ndio inawasumbua watanzania.

Mikataba hii haikufungwa na kina chifu Mangungo bali ilifungwa na wasomi mahiri kabisa na wengine waliosoma vizuri katika vyuo vikubwa kabisa duniani na tena wakilipiwa na wanachi masikini kwa lengo moja tu kubwa, kuwatetea wananchi katika mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Lakini sasa tunachoshuhudia ni kinyume cha yale tuliyoamini, wale tuliowasomesha wamekuwa ni vinara wakubwa wa ufisadi na wamejaa viburi kiasi kwamba mtu anasema hawezi kuachia ngazi/madaraka kwa kelele za wananchi, swali langu hapa ni hili,

Hivi Mtanzania ni nani katika Tanzania!

Friday, January 25, 2008

HE! UNAFIKIRI HII NDIO NJIA SAHIHI?

Wakati wananchi wa sehemu fulani hapa Tanzania waliposikia kuwa 'gavana' ametolewa katika nafasi yake, baadhi ya wanajamii walivamia mashamba yake kilometa chache nje ya mji mkuu wa kibiashara.

Mimi kitendo hiki ninakiona ni cha kipekee kabisa, yaani mtu anapigiwa simu kuwa waende wakagawane mashamba ya fulani kwa kuwa tu huyo fulani ni fisadi! Wapi tunakwenda.

Sina hakika kama yale mwimbaji maarufu na mwanaharakati wa Marekani Tracy Chapman aliyoimba katika REVOLUTION 'mapinduzi ya watu wa chini' yanatimia.

Je!, wasiosema wameanza kusema! au wasiosikia wameanza kusikia, na nini kitafuata endapo mikononi watashika kilichokaribu yao!

Tusubiri
SAKATA LA BOT: WALIO KIMYA NAO WAMEKULA


Sidhani kama kuna yeyote mwenye uchungu na Tanzania anahitaji kuelezwa mwanzo wa mabilioni 133 yaliyotafunwa, kwa taarifa, pale kwenye benki kuu ya Tanzania. Kwa sasa kila mtu anamnyooshea mkono Ballali, gavana ambaye rais Kiwete ametengua uteuzi wake kama gavana.

Kwa maoni yangu, mimi nadhani mtu kama Ballali hawezi kuzitumbua pesa hizo peke yake hata kama angekuwa anakula kama funza. Kawaida ya funza huwa anakula na k****a wakati huo huo na ndio maana funza ni waharibifu wakubwa na mazao ya nafaka.

Hizi pesa zimeliwa na wengi, wengi tena sana ila kwa kuwa Ballali alimuonesha 'mungu' tumbo pale alipokanusha taarifa ya dk Slaa basi ndo leo umma umeamua kumuhukumu, na hakika hata kama atasafishwa vipi bado sisi tunamuona kama fisadi anayestahili kuhukumiwa na kufilisiwa kabisa na kama ndo ingekuwa katika zile nchi za kisoshalisti za kweli basi angeuawa hadjharani baada ya kuwa amewataja mafisadi wenzake.

Namtetea Ballali kuwa hizo pesa hajazila peke yake, amekula na wengi ambao wapo bado madarakani tena wanashikilia nyadhifa kubwa sana zinazowawezesha kusaini mikataba kwa niaba yetu huku wakitanguliza maslahi yao kwani hii ni kawaida yao. Tunaimba pamoja kijamaa wao wanacheza kifisadi.

Wengi waliokula wamekaa kimya huku wakijifanya hawahusiki na tena wengine bado ni 'wajumbe' wa bodi. Tunawasubiri hawa waseme kwa hiari la sivyo umma utawataka waseme wakiwa uchi
AFCON: TUNA MENGI YA KUJIFUNZA WATANZANIA


Tangu mwanzo wa mwaka huu 2008 si kwamba kila mtanzania amekuwa makini kufuatilia mashindani ya Mataifa ya Afrika yanayoendelea katika miji mbalimbali ya Ghana bali kila mtu na mpenzi wa soka duniani amekuwa makini kuna nini kinaendelea huko ambako miamba ya soka la kiafrika inakutana tangu kipite kindi cha miaka miwili ambapo Misri ilitwaa kombe hilo mbele ya 'Tembo' Ivory Coast.

Sitakuwa mchambuzi wa kuelezea mechi ambazo ndo kwanza zinaelekea katika hatua ya robo fainali bali mimi nitajaribu kujikita katika uga ambapo sisi kama watanzania tunaweza kuchota chochote kutoka Ghana.

Hakuna mtanzania ambaye anaweza kusahau namna timu yetu ya taifa ilivyoandaliwa kwa kupewa kila aina ya msaada na seriali ilivyoshindwa kushinda mechi muhimu za nyumbani na hivyo kutukosesha nafasi ya kuwakilisha nchi za jumuia ya Afika mashariki katika AFCON Ghana2008

Kikubwa ambacho ninaweza kuelezea mwanzoni kabisa ni namna ya kuthamini vipaji vya vijana wadogo bila kusahau uzoefu wa wachezaji wenye umri mkubwa lakini unaowawezesha kucheza soka. Pia nafasi ya wataalamu wa soka wazalendo katika kufanikisha mipango ya ushindi na si kushirikia na kutolewa katika hatua za mwanzo.

Tangu awasili kocha aliyetafutwa na serikali toka Brazil wengi tulikuwa na mawazo makubwa ambapo kila mtu alitazamia kabisa kuiona taifa stars ikicheza na kupata nafasi ya kwenda Ghana. Matarajio haya yalionekana kuwa kweli kutokana na namna serikali na wadau wengine walivyojitolea kuisadia timu hii ambayo mwanznoni ilionekana kama imetelekezwa.

Tatizo limejitokeza pale mtaalamu wa kibrazil alipoonesha kuwadharau watanzania akijifanya kuwa wakati alipokuja sisi hatukuwa tukijua mpira wowote na hivyo hatuwezi kumshauri katika kitu kinachoitwa soka. Kung'ang'ania kwake wachezaji chipukizi si vibaya lakini siku zote 'kijiji hakikosi wazee' lakini kuwatupa wazoefu ni tatizo kubwa. Katika safari mara zote ni lazima wawepo wanaoijua njia.

Vijana walioandaliwa vizuri tangu shuleni wana nafasi kubwa sana ya kuwa hodari katika fani nyingi, ni vizuri sasa kwa serikali na chama cha soka kuweka mikakati ili hata hiyo nafasi ya 2010 tuweze kuipata.

Ushauri wa wachezaji wazoefu, makocha wazalendo usidharauliwe. Hawa ni muhimu sana katika maendeleo ya soka letu. Tunashuhudia leo huko Ghana ambako timu nyingi zina nyota vijana wanaoungwanishwa na wakongwe.

Kwa kuwa mashindano bado yanaendelea na nzuri zaidi kwetu kuwa TVT inarusha matangazo 'live' tuna nafasi ya kujifunza mengi

Thursday, October 18, 2007

MAADHIMISHO YA KIFO CHA NYERERE

Juzi chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere kimeungana na watanzania wote kuadhimisha miaka nane tangu kufariki kwa kiongozi wa kwanza wa taifa hili, Mwalimu Julius Nyerere. Sherehe zilikuwa nzuri na zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali akiwamo wazri Kingunge Ngomale Mwiru aliyekuwa mgeni maalum hapa chuoni.

Yaliongewa mengi na tukaoneshwa mengi kuhusu malimu, hakuna aliyepingana nayo. Mada mbalimbali zilizoandaliwa na wahadhiri na wanafunzi zilitolewa katika maadhimisho haya yaliyofanyika kwa siku mbili. Wachangiaji mbalimbali walichangia hii yote ikiwa ni katika kuonesha kuwa kila mmoja anamtambua na kumthamini mwalimu.

Tatizo langu linakuja pale tu wale tuliowategemea kumwonesha mwalimu kama kiongozi wa watanzania wanamwonyesha kama kiongozi wa CCM. Kingunge pamoja na dhamana aliyokuja nayo ya mtumishi wa umma alishindwa kujizuia kutamba kuwa mwalimu ni wa CCM pekee na wanasiasa wanaomwiga wanafanya makosa kwani wao si wanasisisemu.

Kikubwa pia kilichonitatiza ni pale iliposemwa kuwa mwalimu alijali mali na wananchi, hapa naona ni kama tunadanganyana mchana kabisa, ni kweli kwamba mwalimu alijali wanacnhi kwa kutogawa maliasili za nchi.

Wale wanaojidai kuwa mwalimu ni wao leo tunawaona wakiongoza kwa kuuza nchi na utajiri wake, tazama mikataba mibovu inavyosainiwa kila kukicha na pia angalia jinsi mwananchi wa kawaida anavyotaabika kwa bidhaa kuwa ghali huku viongozi na watoto wao wanavyotanua kutokana na kuendekeza matumbo kuliko watu.

Si busara kumuenzi mwalimu kwa kuimba nyimbo zake huku mkicheza ngoma za ubinafsi, ufisadi na mabaya mengine mengi ambayo ni mwiba kwa watanzania, sanamu tu hazitoshi kuonesha kuwa tunamjali mwalimu bali tukumbuke kuwa mwalimu aliona na kuheshimu mali za watanzania na hakutaka kuzitumia kwa manufaa yake binafsi
HE! ETI KISWAHILI SIO LUGHA YA WASOMI!!!??


Kama kuna siku niliyoshangaa basi ni siku ya Alhamisi, tukiwa katika mjadala hapa darasani, nilizuiwa kuchangia mada kwa kuwa tu nilipaswa kuongea kiingereza. Nilikumbushwa kuwa lugha rasmi ya mawasiliano katika vyuo vya elimu ya juu ni kizungu na eti Kiswahili ambacho ni lugha ya taifa huru la Tanzania hakina nafasi kwa wasomi wasiosoma lugha hii kama somo.

Wengi walishangaa, niliamua kukaa na mwenyekiti alinionya kutoongea lugha hii tena, na hasa ninapokuwa darasani. Mwisho sana mhadhiri wa somo alisimama na kuniruhusu kuchangia mawazo yangu katika mada iliyowasilishwa na kundi la pili iliyohusu 'ulinganifu kati mitizamo ya kisiasa mmoja ukiwa ni mtazamo kongwe na mtazamo wa kisasa'

Kikubwa ninachopaswa kuwauliza ninyi wengine ni hiki, Je Kiswahili si lugha ya mawasiliano katika sehemu za elimu ya juu? au ndo nimuamini yule mzazi kule kwetu anayajua kwamba kama huwezi kuongea kizungu wewe si msomi, tena nikakumbushwa tu kuwa Kiswahili si chochote na halafu tunapaswa tujifunze Kichina
NIMERUDI TENA!!!

Mpendwa msomaji wa blogu hii, kwanza naomba uniwie radhi sana kwa kuwa kimya kwa kipindi kirefu. Nilikuwa nimebanwa na majukumu mazito ya masomo, nafurahi kwamba wanajumuia wenzangu wanaoblogu kwa Kiswahili walifanya kile ambacho wote tunahitaji, habari, taarifa, na burudani.

Kubwa zaidi kwa sasa ni kuendeleza kile wenzangu walichonacho na kama unavyojua jukumu la ukurasa huu ni kukuhabarisha na kusikia wewe unasema nini kuhusu mada mbalimbali ambazo ama ntakuwa nimezichokoza ama wewe ndo umeanzisha.

Natambua kabisa yapo mengi sana ya kujadili ambayo magazeti yetu hayana nguvu ya kuvijadili. Kuwepo kwako kutasaidia wengine kufahamu mengi na kuelemika na hivyo kujitambua.

KARIBU SANA

Tuesday, June 19, 2007

SAFARI YA GHANA INAKUJA!!!!

Hata sisi tunaweza. Ndivyo ninavyoweza kusema baada ya timu yetu ya soka inayofundishwa na Maxio Maximo kuifunga timu ngumu ya Bukinabe kwa goli 1-0 katika uwanja wa ugenini (burkinafaso).

Kwa sasa timu yetu si kichwa cha mwendawazimu kama ilivyokuwa imezoeleka hapo mwanzo. Tunaweza. Vijana wamefanya mabo makubwa ambayo kila mtanzania anayapenda. Tumepewa raha na hakuna wa kutuzuia sasa, mwendo mdundo.

Pamoja na hayo napenda kuwasikitikia baadhi ya wachezaji ambao walijiona wao ndo wao na wakawa wanaleta nyodo, sasa wanasaga meno kwani vijana wadogo wanafanya mabo amabyo wote tunayataka.

Nafurahishwa sana na msimamo wa kocha wa kutokubembeleza, huu ni mfano mzuri kwa walimu wazalendo. Tunaweza.

Unamkumbuka Kaseja pamoja na Mgosi walivyotoa maneno ya kipuuzi? yako wapi, Tunaweza bila wao kwani wapo wachezaji kibao vijana na wenye nidhamu ambao wanawajibika kwa taifa si kwa friend s of nini sijui., pumbavu. Kwa sasa wenzao wanapeta tu na jana wamepata shavu bungeni ambako kila mtu anatamani walau aingie. Cheki zawadi walizopata!

Waziri mkuu kawaahidi mambo makubwa sana endapo wataenda Ghana, na nyumba nazo hizo zinakuja yaani kutakuwa na mtaa wa Maksimo. Kitakuwa ni kijiji cha utalii, nami nitatembelea na kupiga picha.

Tunaweza
SAFARI YA GHANA INAKUJA!!!!

Hata sisi tunaweza. Ndivyo ninavyoweza kusema baada ya timu yetu ya soka inayofundishwa na Maxio Maximo kuifunga timu ngumu ya Bukinabe kwa goli 1-0 katika uwanja wa ugenini (burkinafaso).

Kwa sasa timu yetu si kichwa cha mwendawazimu kama ilivyokuwa imezoeleka hapo mwanzo. Tunaweza. Vijana wamefanya mabo makubwa ambayo kila mtanzania anayapenda. Tumepewa raha na hakuna wa kutuzuia sasa, mwendo mdundo.

Pamoja na hayo napenda kuwasikitikia baadhi ya wachezaji ambao walijiona wao ndo wao na wakawa wanaleta nyodo, sasa wanasaga meno kwani vijana wadogo wanafanya mabo amabyo wote tunayataka.

Nafurahishwa sana na msimamo wa kocha wa kutokubembeleza, huu ni mfano mzuri kwa walimu wazalendo. Tunaweza.

Unamkumbuka Kaseja pamoja na Mgosi walivyotoa maneno ya kipuuzi? yako wapi, Tunaweza bila wao kwani wapo wachezaji kibao vijana na wenye nidhamu ambao wanawajibika kwa taifa si kwa friend s of nini sijui., pumbavu. Kwa sasa wenzao wanapeta tu na jana wamepata shavu bungeni ambako kila mtu anatamani walau aingie. Cheki zawadi walizopata!

Waziri mkuu kawaahidi mambo makubwa sana endapo wataenda Ghana, na nyumba nazo hizo zinakuja yaani kutakuwa na mtaa wa Maksimo. Kitakuwa ni kijiji cha utalii, nami nitatembelea na kupiga picha.

Tunaweza

Saturday, June 16, 2007

NIPO NDANI YA NYUMBA

Wasomaji wangu kwanza kabisa ningependa kuwaomba samahani kwa kupotea ghafla, nilibanwa na masomo na mitihani ilikuwa inakuja wanguwangu. Sio neno kwa sasa nipo mapumziko na najua tutakuwa pamoja katika kujadili mambo ya utamaduni, siasa na uchumi bila kujali yale yote yanayojiri na kuhusisha maisha yetu

Sunday, April 29, 2007

SIMBA NI KIBOKO

Katika ligi ndogo ya soka inayoendelea Tanzania timu ya Simba ndiyo klabu pekee ambayo kipa wake Mustafa ndiye kipa pekee ambaye hajaokota mpra katika nyavu anayoilinda ukiacha magoli ya 'TFF' waliyopewa timu ya Ashanti

Kwa utendaji huu wa tiefuefu nadhani kazi bado ipo kwani hakuna haja ya wao kama chama cha soka kufanya kazi kwa ushabiki tena katika ligi hii ndogo ammbayo haina mwenyeji wala mgeni. Kumfungia mechi sita Golota kwa upande wangu si halali kwani kosa moja katika soka haliwezi kuzaa adhabu kubwa namna hiyo
CHESII YAKARIBIA FAINALI YA UEFA

Klabu bingwa ya soka Uingereza majuzi iliweza kuilaza timu ya livapuli kwa bao moja bila majibu katika uwanja wake wa nyumbani Stamford Bridge.

Bao hilo lilifungwa na winga teleza Joe Cole baada ya kupata pande safi kutoka kwa mwanasoka bora wa Afrika na nyota anayeongoza kwa kupachika mabao katika primia ligi Didier Drogba.

Hii ni hatua kubwa sana katika kuelekea finali na endapo jumanne katika mechi ya marudiano chesii watashinda basi ndoto za Mourhino ya kutwaa kombe zitatimia.

Kumbuka kuwa nyota wa Ghana Michael Essien atacheza katika mechi hii japo kuna shaka ya mlinzi 'kavalo' amabye aliumia wakati wa sare ya ligi dhidi ya Bolton jana

Wednesday, April 18, 2007

CHEKA KIDOGOOOOO!!!

Nimetumiwa na rafiki yangu si vibaya nawe ukasoma( hakuna ubaguzi)


Kuna muhindi mmoja alivamiwa na majambazi kwa bahati akawahi kujificha darini yeye na mkewe kwa kuogopa kuuwawa. Sasa wakawa wanamtaka ashuke la sivyo watavunja kila kitu ndani.

Mhindi akajibu: " Kama tavunja mavitu tanunua mengine lakini hapana shuka

Jambazi: Shuka la sivyoo tutachukuwa pesa zako zote
Mhindi: Kama machukua pesa tapata mengine toka Bombei

Jamabazi: Shuka kama utaki tutauwa watoto wako hapa chini !
Mhindi: Kama mauwa matoto hapana tabu tategneza mengine mashine yote bili iko juu hapa (YEYE NA MKEWE)

UMEYAONA MABANGO WALIYOBEBA WASOMI WA UDSM WALIOSIMAMISHWA!!!!

Nimeingia katika blog ya Michuzi na kujionea mabango ambayo wanafunzi wa mwaka wa kwanza udsm waliandika wakishinikiza mkopo uwe 100%. Tazama hapa pembeni kushoto na bonyeza Michuzi, utajionea picha mbalimbali zilizopigwa kwa uzuri kabisa na gwiji la blog za picha nchini. Baadhi ya mabango hayo yanasema:-

SERIKALI PUNGUZENI SIASA KATIKA MASUALA YA MSINGI MNAUA ELIMU

KIKWETE UMESOMA BURE LEO UNATUDAI40%

KIKWETE BAADA YA WAKULIMA KUKUCHAGUA NDIVYO UNAVYOWALIPA

NASI TUUNDIWE KAMATI KAMA YA MALIMA NA MENGI halafu tupewe Milioni 100

Yapo mengi lakini haya ndo yamenivutia

MGOMO WA CHUO KIKUU, NANI ANAFAIDIKA!!!

Katika kikao chake maalum cha 172 kilichofanyika tarehe 17 april,2007 Baraza la chuo kikuu cha dar es salaam kiliamua kuwasimamisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaosoma udsm pamoja na vyuo vishiriki kwa kushiriki katika mgomo'haramu' wa kupinga malipo ya 40%.Wanafunzi hawa wamesimamishwa masomo kwa muda usiojulikana.

Serikali makini hutumia rasilimali zake katika kuhakikisha kuwa inajenga na kuelimisha vijana ili waweze kuwa na manufaa kwa jamii na serikali yote. Vijana huandaliwa kuja kuwa watu makini na maandalizi haya yana gharama zake amabazo wakati mwingine kama mtu binafsi hawezi kuzibeba na kukidhi gharama hizi.

Nchi zetu nyingi za kiafrika zimekumbatiwa na umaskini ambao si wa mali wala watu bali umaskini wa mawazo ya kupanga nini kipewe kipaumbele kwa ajili ya kuleta maendeleo ya kesho na si kujineemesha leo na kutaka sifa sizo maana.

Serikali zetu nyingi zimekuwa zikitenga fungu kubwa sana kwa ajili ya ulinzi na IKULU huku sekta nyingine zikipewa kiduchu. Sipingani na kutoa vingi kwa ajili ya ulinzi lakini nashindwa kujizuia kujiuliza kwamba sisi Tanzania adui yetu ni nani na kwanini IKULU itumie pesa nyingi saaaana kwa kipindi kifupi!?

hakuna kitu muhimu kama elimu, haijalishi kama ni elimu ya kujitambua ama ni elimu ya kukariri ili upate cheti huku ukishindwa kujitambua. Kujitambua mara zote huanzisha safari moja.

Siwaungi mkono waliogoma kwani naamini kabisa kuna njia nyingine ambazo wangechukua ili kupata haki yao (ambayo hata mimi ninaihitaji). Wengi wa wanafunzi(nikiwamo mimi) tunatoka vijijini na nauli yakutufikisha chuoni hubidi upitishwe mchango, sasa serikali inapotoa mkopo ambao haukidhi mahitaji na bado haikubali kuwa ndani ya nchi kuna matabaka hivyo wengine wanapaswa kupewa zaidi ya wengine na wengine kunyimwa kabisa(hebu wafikirie watoto wa vigogo ambao wamesoma shule za kulipa mamilioni ambao nao wazazi wao wanataka wapewe pesa zinazotustahili makabwela!)

Suala la matumizi ya anasa ya baadhi ya ofisi za umma na watendaji wa umma linachangia sana katika kutengwa kwa vitu muhimu vya kutimizwa.

Najua watu wengi wnawalaumu wanafunzi wa udsm kwa mgomo, lakini kujitambua ni hatua kubwa katika maendeleo hata kama namna ya kuyaleta itaumiza.

Ni lazima kuwepo na vipaumbele katika vitu muhimu hasa suala la elimu ya juu na ya ufundi ili kujenga taifa endelevu. Masuala ya baadhi ya ofisi kutumia pesa za walalahoi kwa ajili ya manufaa yao hayafai katika nchi hii. Tubadilike na tujitambue huku tukiweka ubinafsi, unafiki na ubabzazi pembeni ili tuendelee mbele. Mgomo ulisitahili na mkopo ni budi utolewe kwa wahitaji kwa 100%

Wednesday, April 11, 2007

PASAKA BILA PILAU LA NG'OMBE!!!

Kama kuna sherehe ambayo iliwaweka watu wote katika mstari basi ni hii ya pasaka ya mwaka huu. Yaani ilikuwa ni mchicha na kuku kwenda mbele kisa ni RVF.

Thursday, April 05, 2007

JE, DINI NA MUNGU WA WAAFRIKA NI MSHENZI?
Na: Obe Mashauri

Habari hii niliiandika mwaka 2003 na ilitoka katika gazeti la Uhuru, ilihaririwa sana. Nimeona nikupatie uisome kama nilivyokuwa nimeiandika

Ni falsafa ya uongo kwa mtu kuamini kwamba waafrika hawakuwa na dini kabla ya kuja kwa wageni waliokuja kwa nia ya kupora utajiri wa bara hili.
Dini ni njia ya kuhusiana na Mungu. Kwa tafsiri hii ni uongo wenye kutu kusema kwamba kabla ya wazungu na waarabu kutuvamia tulikuwa watu wasio na diniau kwa lugha nzuri kwao nakwa wafuasi wao wa sasa, wapagani au makafiri.
Wengi wetu tumekuwa tukiamini kwa kuaminishwa kwamba dini zilizoletwa na wageni ndiyo dini za asili.ukoloni na utumwa wa maharamia hawa ulitufanya tuamini kwamba Mungu wa majangiri hawa ni wa kweli. Mungu aliyeabudiwa na wenyeji aliitwa mshenzi na mitume wake wakaitwa mapepo. Huu ndio ustaarabu wa wageni.
Baada ya kuwa zimejikita afrika kwa mabavu na propaganda, zimewajaza wafuasi wake falsafa mpya ya kujibagua na kujiona bora zaidi ya wengine
Tanzania na afrika kwa ujumla katika miaka ya hivi karibuni imeshuhudia vujo na migogoro mikubwa ya kidini inayoletwa na dini hizi za ukristo na uislam katika ama kujitanua au kujiona bora zaidi ya nyingine.
Mbaya zaidi migogoro baini ya dini hizi inawaathiri hata wasiozifuata. Mambo haya hayakuwahi kutokea kutoea kabla ya kuja kwa dini hizi za kigeni.
Historia ni shahidi wa mengi. Historia ya mwafrika haioneshi machafuko au vita vilivyosababishwa na dini za asili. Dini ambazo ‘wakoloni na mabwana’ waliziita za kishenzi huku waumini wake wakibatizwa majina kama wapagani,kaffir na majina mengine mengi ya kipuuzi.
Ukristo na uislamu ni dini za kibiashara zenye historia ya vita katika kujitanua. Itkadi ya dini hizi ilisambazwa kwa heri au shari kwao waliozikataa. Walikuwa wakimtangaza Mungu wao kwamba ndiye wa kweli na hapana mwingine ila yeye.
Ukristo na uislam uliokumbatiwa na waafrika uliletwa afrika si kwa minajili ya kumtangaza mungu wa kweli bali dini hizi zilikuwa ni mbinu za wazungu na waarabu kujitanua kiuchumi na kisisasa katika bara hili tukufu. Biashara ya utumwa na ukoloni vinadhihirisha haya.
Kwa mantiki hii utaona kwamba mungu anayehubiriwa katika dini hizi ni yule anayehalalisha uporaji na uuwaji wa watu wasiomtaka.
Uislamu ulisambazwa kwa upanga mkali uliokata shingo na viungo kwa wote walioukataa. Jitihada zilizofanywa na uthman dan fodio zinadhihirisha jambo hili.
Mabomu,mishale, risasi na uongo nazo zilitumika kuusimika ukristo na yule aliyeukataa aliitwa msaliti, kifo ni zawai yake.
Mtu aliyepingana na dini hizi aliuawa.
Falsafa iliyopandikizwa na wakristo na waislam vichwani mwa waafrika bado inatutawala mpaka sasa. Ukweli ni kwamba kila mtu ana Mungu wake anayeujua utamaduni wake na kila hali yake ya maisha ya kila siku.
Kwa waafrika Mungu huyu alijulikana kwa majina anuai, wapo waliomwita Ngai, Mulungu, Lyoka na majina mengine mengi yanayoonyesha utukufu wake.
Dini za kiafrika ziliabudu Mungu mmoja tu na si kwamba wageni ndio waliowaletea waafrika dini na kuwatambulisha kwa Mungu. Ustaarabu ulikuwapo afrika na wazungu na waarabu ndio waliokopi ustaarabu huu.
Dini za kigeni ziliudharau utamaduni wa mwafrika na kumtambulisha kwa utamaduni mpya wa kujidharau na kudharau kila kilicho chake, akiiponda dini yake na kukumbatia ukisasa eti huo ndio ustaarabu.
Kwa kuudharau utamaduni wake mwaafrika amekuwa kama kasuku, kazi yake ni kuimba kila anachopewa na bwana wake. Lugha za kiafrika karibuni zitatoweka kwa kuwa tu hazina nafasi katika dunia ya wastaarabu. Lugha muhimu ni kizungu na kiarabu tu.
Ukitaka kumtawala mtu basi mporeulimi wake. Majangiri hawa wamefanikiwa kwa hilo. Kwani kila mtu hata kuamini ukisema umetokewa na Mungu anayeongea lugha yako. Wao Mungu ni yule anayeongea kwa lugha zao,Mungu asyeongea lugha zao basi watamwita shetani kama ilivyotokea Joan of the Arc huko London. Kitabu cha the African civilization kinalieleza hili.
Mwanzoni mwa muongo huu watanzania tumekuwa tukishuhudia migogoro na fujo nyingi za kidini zikitokea na ukijaribu kuchunguza kwa umakini migongano hii imekalia katika maslahi binafsi ya dini hizi na si kumtangaza mungu wao.
Machafuko haya yanayotokea ndiyo yanayonifanya nijiulize kama kweli dini zetu zilikuwa za kishenzi?
Hivi matusi, vita, migongano na machafuko yanayotokea katika nyumba za ibadandio ustaarabu tulioletewa?
Hivi wageni hawa walituletea Mungu tuliyemjua sisi au mungu wao mpenda vita, mwenye wivuna mbaguzi? Je, ni kweli kwamba sisis hatukuwa na Mungu? Swali hili nisingependa waljibu wasomi waliokaririshwa kwamba cha mzungu na mwarabu ndio bora
Kama tusingekuwa na Mungu ‘wastaarabu’ hawa wangetukuta kweli? Moyo wa ukarimu tuliowaonyesha japo walitutemea mate, ulitoka kwa Mungu wa kishenzi kweli? Hivi Mungu wetu aliyetulinda na kutupa akili ya kumjua alikuwa ni Mungu aliyevaa ngozi ya kondoo.
Je, mungu aliyeruhusu wengine kupora,kutawala kwa mabavu na kuuza binaadamu kama bidhaa ndiye mungu wa kweli?
Maswali haya pamoja na hili linalosema kwamba ukristo na uislam ni dini za ulimwengu (universal) yananifanya nijiulize na kuchoshwa na hadithi za vitabuni.
Ukweli usiolazimishwa kuukubali ni kwamba dini hizi mbili si dini za ulimwengu kama tunavyopotoshwa. Kwa afrika dini hizi ni ngeni kabisa na hatukuwa na migogoro ya kidini kama tunayoishuhudia sasa katika dini hizi ngeni.
Ni wakati wa waafrika sasa kurejea katika imani ya asili tuliyokuwa nayo, imani inayotutambua sisi na utamaduni wetu. Turudi katika dini zetu ili tutunze ustaarabu wetu, utamaduni wetukila fahari yetu.
Dini zetu za jadi ndizo zitakazotuepusha na migogoro tunayoishuhudia sasa na kwa bahati mbaya sana tunaishiriki tu eti kwa kuwa tumebatizwa na kusilimishwa katika majina mapya tusiyojua maana yake.
Vilevile tujue dini hizi mwanzo wake na wafuasi wake wa mwanzo. Ukristo ulianzishwa na kikundi cha waalimu (rabbi) Yesu akiwa mwanzilisha wakati Uislamu ulianzishwa na mfanyabiashara aliyeitwa Muhamad aliyejiita mtume huko mashariki ya mbali na kuusambaza kwa vita akianzia huko Makka.
Kuzifuata na kuzikubali dini hizi ni kukubaliana na waanzilishi wa dini hiziz na misemo yao kama…ya kaisari mpe kaisari…., na bakora ndizo zitakazoleta usuluhishi kati yetu!
Kukataa kurudia dini zetu ni kukumbatia laana tulizopata kwa kuaminishwa kwamba waafrika hatuna Mungu
Ufumbuzi wa migogoro tunayoishuhudia katika dini za kigeni ni kurudi katika dini zetu za asili zinazotutambua kwamba sisi ni nani na ni kwa ajili ya nani.
Tumekuwa na tunakuwa wanyonge kwa kukumbatia dini hizi zinazotunyima uhuru wa kuhoji kwani mafundisho yake yanatumia lugha tusizozielewa na zinatokana na mawazo ya watu wenye utamaduni tofauti na wetu.
Tujiuliza kama zingekuwa ni dini za kweli mbona zinabaguana na viongozi wa dini hizi wanajiona wao ni bora kuliko waumini wake.
Ukweli hata ukipingwa haubadiliki kuwa uongo. Ukweli ukishindwa ni kama umesakafiwa tu na siku moja utaibuka na waliopinga wataficha nyuso zao kwa aibu

Monday, April 02, 2007

SULUHU KAMA USHINDI VILE......

Lilikuwa ni bao la kusawazisha liliofungwa kipindi cha pili muda wa lala salam ndilo lililobadilisha matokeo na kuiokoa timu ya chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere isiadhirishwe na chuo cha ustawi- Kijitonyama.

Mechi hiyo iliyofanyika katika uwanja wa MNMA ilishuhudia timu ya MNMA ikiwa ya kwanza kupachika bao lililofungwa na mshambuliaji mahiri Magesa dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza na hivyo kuamsha ari kwa wachezaji na washangiliaji waliokuwa wamejazana kwa wingi kuisapoti timu yao ambayo haina rekodi nzuri ya kushinda mechi inazocheza katika uwanja wake wa nyumbani.

Hatahivyo Ustawi walisawazisha kabla ya mapumziko. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Ustawi wakifunga bao 'tamu' la luninga lililofungwa na mshambuliaji mwenye jezi namba9mgongoni. Bao hili liliwachanganya wachezaji na mashabiki pia huku wakijikuta wakirejea kumbukumbu za timu ya taifa kufungwa na simba wa teranga. Lakini alikuwa ni Marijani aliyefuta ndoto za wageni kuongoza baada ya kusawazisha goli baada ya kupokea pasi safi toka kwa winga mahiri Joshua 'basopa'.

Mpira huu ulioshuhudia kazi kubwa kati ya mshambuliaji wa Ustawi na beki wa pembeni wa MNMA Allain, ulitawalaliwa na rafu za kimchezo huku mwamuzi akijitahidi kuumudu mchezo. Ustawi walipata bao la tatu baada ya kiungo mchezaji jezi namba14 alipounganisha krosi safi toka winga ya kushoto. Lakini ni Ayub Denge maarufu kama Jobe ndiye alieleta faraja kubwa kwa MNMA baada ya kufunga bao la shuti lililomshinda kipa wa Ustawi na kuleta furaha kubwa kwa mashabiki wa MNMA.

Hadi mwisho wa mchezo timu zote zilitoka nguvu sawa. Baada ya pasaka timu ya MNMA inataraji kucheza na timu ya IFM

Timu ya MNMA iliwakilishwa na
1 SWEDI
2 Allen (
3 Maximilian
4 MUDI
5 Father
6 RASHIDI
7 Baseke
8 Mungai
9 Hamad (Marijani)
10. Jobe
11 Magesa(Joshua)
RVF: KILA MMOJA ANAJIDAI ETI YE'VEJETARIANI'

Homa inayoogopwa kabisa kwa sasa imeingia dar. Inaogopwa kwa sababu inapatikana katika kitoweo tena kitoweo chenyewe kikiwa ni nyama ya ng'ombe. Homa hii kitaalamu imepewa jina la Rift Valley Fever ama kwa kiswahili homa ya bonde la ufa.

Hapa chuoni kwa sasa kila mtu amejipachika 'urasi' kwamba yeye si mtu wa nyama bali ni matunda na mboga za majani. Ukienda kafteria chakula kinacholiwa sana ni ugali ama wali na mbogamboga ambazo hata hivyo zimepikiwa mafuta ya wanyama.

Labda tueleweshwe zaidi kuhusu hii homa, hivi haya mafuta ya wanyama hayana HBU